Kaimu mkuu wa mkoa wa Morogoro 
ambaye ni mkuu wa wilaya ya Mvomero, Anthony Mtaka akikabidhiwa zawadi 
ya fulana  na Mkurugenzi wa uhusiano na sheria wa TBL, Steven Kilindo 
yenye ujumbe wa wiki ya nenda kwa usalama barabarani baada ya mkuu huyo 
kuzindua rasmi upimaji wa afya kwa madereva wa mabasi na malori ya 
masafa marefu katika kituo cha mizani cha Mikese mkoa wa Morogoro, zaidi
 ya madereva 200 wanatarajiwa kupimwa afya katika vituo vya Mikese 
Morogoro, Mkata mkoani Pwani na Makuyuni mkoani Arusha. katikati ni 
Mganga mkuu wa macho wa jeshi la polisi Dk Charles Msenga na kulia ni 
kaimu mkuu wa usalama barabarani mkoa wa Morogoro, Willie Mwamasika
 Mganga
 mkuu wa macho wa jeshi la polisi Dk Charles Msenga kulia akimpima uwezo
 wa kuona macho dereva wa kampuni ya usafirishaji wa abirianya Abood 
basi Morogoro, Augustino Mpepwa wakati wa uzinduzi wa afya kwa madereva 
wa mabasi na malori ya masafa marefu ikiwa sehemu ya uzindui wa wiki ya 
nenda kwa usalama barabarani katika kituo cha mizani cha Mikese mkoa wa 
Morogoro, zaidi ya madereva 200 wanatarajiwa kupimwa afya katika vituo 
vya Mikese Morogoro, Mkata mkoani Pwani na Makuyuni mkoani Arusha.
 DK YOHANA KIBONA KUMPIMA DC ANTHONY MTAKA AFYA KULIA NI DK CHARLES MSENGA MGANGA WA JESHI LA POLISI MAKAO MAKUU 
DR YOHANA KIBENA akiwaandikisha 
madereva tayari kupimwa afya zao katika Hospitali ya Polisi ya Morogoro.
 TBL imefadhili upimaji wa afya hizo.
No comments:
Post a Comment