SERIKALI
 inatambua na kuthamini mchango wa sekta ya hifadhi ya jamii nchini hasa
 katika kusaidia kukuza na kuimarisha uchumi na kuinua hali za 
watanzania kwa ujumla hasa wale wanaofikiwa na huduma hizo.
Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa
 Mkoa wa Tanga,Salum Chima wakati akifungua semina ya mfuko wa Pensheni 
wa PPF kwa maafisa wa makampuni mbalimbali katika (Kanda ya 
Kinondoni)mkoa wa Tanga.
Amesema kuwa serikali inatambua kuwa huduma ya hifadhi ya jamii inawafikia watu wachache sana licha ya umuhimu wake kwa jamii.
Aidha amesema kuwa kwa kutambua 
umuhimu huo serikali imekuwa ikiimarisha sekta hiyo ili iwez kupanua 
wigo wa watu wanaonufaika na huduma hiyo kwa kurekebisha sheria na 
kuweka mazingira bora kwa watu wote wanaojiunga na mfuko huo.
Alifurahishwa kusikia kuwa mfuko 
wa Pensheni wa PPF ambayo ilianzishwa mwaka 1978 kwa ajili ya pensheni 
za mashirika ya umma lakini pia kisheria inaweza kusajili hata makampuni
 binafsi,taasisi za elimu na vyuo binafsi,taasisi za dini na 
waliojiajiri wenyewe ikiwemo walioko kwenye sekta isiyo rasmi.
Amesema kuwa hatua hiyo itawafanya
 watanzania wengi zaidi waweze kupata huduma bora za mfuko wa PPF na 
kuwa na uhakika ya maisha bora ya sasa nay a baadae kama iliyokuwa kauli
 mbiu ya PPF.
Kwa upande wake,Meneja wa PPF 
Kanda ya Kinondoni,Pwani na Tanga,Zahra Kayugwa amesema kuwa 
watawapeleka mahakamani waajiri wote ambao watakuwa hawawasilishi 
michango ya wafanyakazi wao kwa wakati.
No comments:
Post a Comment