TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, September 26, 2014

”SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI SEKTA ZA HIFADHI YA JAMII NCHINI”

FSERIKALI inatambua na kuthamini mchango wa sekta ya hifadhi ya jamii nchini hasa katika kusaidia kukuza na kuimarisha uchumi na kuinua hali za watanzania kwa ujumla hasa wale wanaofikiwa na huduma hizo.
Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Salum Chima wakati akifungua semina ya mfuko wa Pensheni wa PPF kwa maafisa wa makampuni mbalimbali katika (Kanda ya Kinondoni)mkoa wa Tanga.
Amesema kuwa serikali inatambua kuwa huduma ya hifadhi ya jamii inawafikia watu wachache sana licha ya umuhimu wake kwa jamii.
Aidha amesema kuwa kwa kutambua umuhimu huo serikali imekuwa ikiimarisha sekta hiyo ili iwez kupanua wigo wa watu wanaonufaika na huduma hiyo kwa kurekebisha sheria na kuweka mazingira bora kwa watu wote wanaojiunga na mfuko huo.
Alifurahishwa kusikia kuwa mfuko wa Pensheni wa PPF ambayo ilianzishwa mwaka 1978 kwa ajili ya pensheni za mashirika ya umma lakini pia kisheria inaweza kusajili hata makampuni binafsi,taasisi za elimu na vyuo binafsi,taasisi za dini na waliojiajiri wenyewe ikiwemo walioko kwenye sekta isiyo rasmi.
Amesema kuwa hatua hiyo itawafanya watanzania wengi zaidi waweze kupata huduma bora za mfuko wa PPF na kuwa na uhakika ya maisha bora ya sasa nay a baadae kama iliyokuwa kauli mbiu ya PPF.
Kwa upande wake,Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni,Pwani na Tanga,Zahra Kayugwa amesema kuwa watawapeleka mahakamani waajiri wote ambao watakuwa hawawasilishi michango ya wafanyakazi wao kwa wakati.

No comments:

Post a Comment