Wahitimu
 wa kidato cha nne, Shule ya Sekondari Lilasia, iliyopo eneo la Kitunda 
kwa Kibeberu, Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja na wadau 
mbalimbali wa shule hiyo, kwenye sherehe ya mahafali ya sita 
iliyofanyika Dar es Salaam jana.Mwanafunzi  wa Shule ya Sekondari 
Lilasia, iliyopo eneo la Kitunda kwa Kibeberu, Dar es Salaam, Beatha 
Shembilu, akipokea cheti cha kuhitimu kidato cha nne kutoka kwa mgeni 
rasmi, Samwel Lyimo, katika sherehe za mahafali ya sita ya shule hiyo, 
zilizofanyika Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkurugenzi wa Shule hiyo, 
Christina Lyimo, na Mkuu wa Shule, Silas Kamando. Wanafunzi wa Kidato 
cha Nne nchini kote wanatarajia kuanza mitihani yao ya Taifa ifikapo 
Novemba 3 mwaka huu. 
Mwanafunzi 
 wa Shule ya Sekondari Lilasia, iliyopo eneo la Kitunda kwa Kibeberu, 
Dar es Salaam, Flora Jeremiah, akipokea cheti cha kuhitimu kidato cha 
nne kutoka kwa mgeni rasmi, Samwel Lyimo, katika sherehe za mahafali ya 
sita ya shule hiyo, zilizofanyika Dar es Salaam jana. Kulia ni 
Mkurugenzi wa Shule hiyo, Christina Lyimo, na Mkuu wa Shule, Silas 
Kamando. Wanafunzi wa Kidato cha Nne nchini kote wanatarajia kuanza 
mitihani yao ya Taifa ifikapo Novemba 3 mwaka huu. 
Mwanafunzi 
 wa Shule ya Sekondari Lilasia, iliyopo eneo la Kitunda kwa Kibeberu, 
Dar es Salaam, Peter Nyaikobe, akipokea cheti cha kuhitimu kidato cha 
nne kutoka kwa mgeni rasmi, Samwel Lyimo, katika sherehe za mahafali ya 
sita ya shule hiyo, zilizofanyika Dar es Salaam jana. Kulia ni 
Mkurugenzi wa Shule hiyo, Christina Lyimo, na Mkuu wa Shule, Silas 
Kamando. Wanafunzi wa Kidato cha Nne nchini kote wanatarajia kuanza 
mitihani yao ya Taifa ifikapo Novemba 3 mwaka huu. 
 
Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari Lilasia, Christina Lyimo.
Shule ya Sekondari Lilasia yafanya mahafali ya 6.
*Wataka kuwe na lugha maalum mashuleni
NA ANDREW CHALE
NJIA nyepesi ya kukabiliana na 
tatizo kubwa la ajira kwa vijana nchini ni kuongeza kasi ya uwekezaji 
kwenye viwanda, sanjari na kuutazama upya mtaala wa kufundishia kuanzia 
shule za msingi hadi vyuo vikuu, hususan kwenye eneo la lugha, imeelezwa
Akizungumza kwenye mahafali ya 
6, ya Shule ya Sekondari Lilasia, iliyopo Kitunda, Dar es Salaam jana 
septemba 20, Mkurugenzi wa shule hiyo, Christina Lyimo, alisema kupitia 
viwanda vijana kwa maelfu yao wataajirika na kujiajiri kwa mtiririko wa 
fursa zitakazokuwepo, huku pato la taifa likizidi kukua.
“Sina shaka sana na rasilimali 
tulizonazo..zinatosheleza, tuna uchumi mkubwa, hebu kama serikali 
itanisikia niombe sasa tuwekeze nguvu kwenye viwanda, tupeleke surveyors
 wakapime maeneo, sababu tuna nguvu kazi kubwa, tuna rasilimali..tuanzie
 hapo,” alisema Lyimo.
Aidha, Lyimo, ambaye kitaaluma 
ni mwalimu anayehudumu kazi hiyo kwa zaidi ya miaka 25 sasa, ameshauri 
yafanyike mabadiliko ya mtaala hususan kwenye lugha ya kufundishia, huku
 akisisitiza ni wakati mwafaka sasa kwa taifa kuamua ni lugha ipi 
itumike kufundishia kama ni Kiingereza au Kiswahili, tofauti na ilivyo 
sasa kuchanganya changanya.
“Watoto wengi wanababaika kwenye
 mitihani kwa sababu ya Lugha..watoto wengine wanafeli kwa kushindwa 
kujieleza kwa lugha za kigeni!..shule ya msingi Kiswahili miaka 
saba..sekondari kiingereza kwa kweli inachanganya, tuamue basi 
kubadilisha kama ni medium basi ziwe kuanzia awali hadi vyuo vikuu, na 
kadhalika kama Kiswahili iwe hivyo,” alisema
Hata hivyo, katika hatua 
nyingine, aliwaomba wafadhili kujitokeza kuchangia shule hiyo kwenye 
eneo la upatikanaji wa maabara ya kisasa, ikizingatiwa shule kwa sasa 
pamoja na mambo mengine inasomesha watoto yatima bure na kusaidia kwa 
kiasi utoaji wa elimu bora kwa watoto wa Kitunda na kwingineko nchini
“Tunaomba pia serikali igeuzie 
macho kwenye shule hii, tuna watoto yatima hapa, itusukume kwenye kupata
 ruzuku sababu tunasaidia taifa na hata ada tunazopokea ni ndogo mno,” 
alisema
Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya
 Lilasia, Silas Kamando alisema katika mahafali hayo jumla ya wanafunzi 
36 wakiwemo wanaume 17 na wasichana 19 wamehitimu kidato cha nne mwaka 
huu, na kwa sasa wanajiandaa na mtihani wao wa taifa unaotarajia 
kufanyika Novemba 3 mwaka huu, nchini kote.
No comments:
Post a Comment