Mwanamme
 mmoja raia wa Uturuki aliyempiga risasi na nusura amuue aliyekuwa 
kiongozi wa kanisa katoliki papa John Paul wa pili mwaka 1981 ameweka 
maua kwenye kaburi lake katika makao makuu ya kanisa katoliki ya 
Vatican.
Ziara ya Mehmet Ali Agca kwenye makao ya Vatican 
inafanyika miaka 30 tangu John Paul amtembelee gerezani na kumsamehe kwa
 kujaribu kumuua.
Bwana Agca aliomba kukutana na kiongozi wa sasa wa kanisa katoliki papa Francis lakini hata hivyo ombi lake lilikataliwa
Aliachiliwa
 kutoka gerezani nchini Italia mwaka 2000 na kisha baadaye akatumikia 
kifungo chengine cha miaka 10 nchini Uturuki kwa makosa tofauti.
Hadi sasa sababu zake za kutaka kumuua papa John Paul hazijulikani.

No comments:
Post a Comment