TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, December 28, 2014

Malaysia:Waziri mkuu akatiza ziara

Mafuriko nchini Malaysia
Waziri mkuu nchini Malaysia amesitisha ziara yake nchini Marekani na kurejea nyumbani kuweza kutembelea maeneo yaliyoathiriwa na janga la mafuriko mabaya tangu miaka kumi iliyopita.
Uamuzi huo wa Najib Razak unafanyika baada ya shutuma dhidi ya serikali kwa kukosa kutangaza hali ya hatari kwenye majimbo matano yaliyo kaskazini mashariki mwa nchi.
Kupanda kwa haraka kwa viwango vya maji kumewalazimu zaidi ya watu 100,000 kuhama makwao.
Watu watano waliuwa.
Waziri mkuu aliyekuwa akicheza gofu na rais obama akatiza ziara yake nchini humo ili kushungulikia mafuriko nchini mwake
Mvua zaidi inatarajiwa kunyesha katika maeneo ya kusini mwa nchi saa zinazokuja.
Bwana Razak alishutumiwa baada ya picha zake alizokuwa akicheza gofu na rais wa Marekani Barack Obama kusambaa mitandaoni.

No comments:

Post a Comment