MFUKO wa Pensheni wa PSPF 
umedhamini mchezo wa kirafiki utakaowakutanisha wachezaji waliowahi 
kuwika katika timu kongwe nchini Simba na Yanga.
Mchezo huo unatarajiwa kufanyika tarehe 1 Januari 2015 katika 
uwanja wa chuo cha Bandari, Tandika jijini Dar es Salaam, kiingilio 
kitakuwa bure ikiwa ni zawadi ya mwaka mpya kutoka PSPF. 
Katika mchezo huo baadhi ya wachezaji wa Simba wanaotarajiwa 
kushuka uwanjani ni Thomas Kipese, George Lucas, Bita John, George 
Masatu, Mustafa Hoza, Emmanuel Gabriel, Idd seleman. Timu ya Simba 
inafanya mazoezi katika uwanja wa Leaders uliopo Kinondoni, ipo chini 
kocha mchezaji Kasongo Athuman. 
Wanaotarajiwa kushuka uwanjani kwa upande wa Yanga ni Peter 
Manyika, Mwanamtwa Kihwelo, Edibily Lunyamila, Mohamed Husein, Chibe 
Chibindu, Aboukar Salum, Bakari malima. Yanga wanafanya mazoezi katika 
uwanja wa kauda ulipo katika makao makuu ya klabu hiyo kariakoo Jijini 
Dar es Salaam, wakiongozwa na kocha Peter Tino.
Lengo la mchezo huo ni kutoa burudani kwa wakazi wa Jiji la Dar 
es Salaam na maeneo ya karibu hususani katika kipindi hiki cha sikukuu 
za mwisho wa mwaka. PSPF itatumia fursa hiyo kutangaza huduma zake mpya 
ambazo Mkopo wa Elimu na Mkopo wa Kuanza Maisha. Tunatoa mwito kwa 
wapenzi wa soka kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo ili kuwaona 
wakongwe waliowahi kutikisha nchi katika anga ya soko nchini.

No comments:
Post a Comment