Miss Tanzania Lilian Kamazima (kulia) akiwa na watoto katika kituo cha New Life cha Boko.
Miss Tanzania Lilian Kamazima 
(kulia) akimkabidhi zawadi ya mwaka mpya Msimamizi wa kituo cha kulelea 
watoto yatima cha New Life kilichopo Boko, Mwanaisha Magambo kwa ajili 
ya watoto 102 waliopo kituoni hapo, tukio hilo lilifanyika juzi.
Miss Tanzania Lilian Kamazima 
(kushoto) akiwa na Miss Kinondoni Maria Shila wakiwa wamembeba mtoto 
aliekuwa kwenye kituoo cha kulelea watoto yatima cha New Life cha Boko, 
mtoto huyo alifikishwa hapo akiwa na siku nne tu tangia kuzaliwa kwake
………………………………………………………………………….
Redds Miss Tanzania 2014 Lilian 
Deus Kamazima jumapili iliyopita alitoa misaada ya vyakula vya aina 
mbalimbali kwa kituo cha New Life Orphans Home kilichopo eneo la Boko 
nje kidogo ya jiji la D’salaam.
Kituo hicho ambacho kilianzishwa 
mwaka 2005 awali kilikuwa maeneo ya magomeni makuti kilianza na watoto 
yatima 17 na baadae kuongezeka hadi kufikia 70. Na kulazimika kuhama 
eneo hilo na kuhamia kigogo ambapo waliishi eneo hilo hadi hivi karibuni
 walipopata mfadhili mmoja kutoka nchini Qatar ambaye amewajengea jumba 
moja kubwa na la kisasa eneo la Boko Dawasa, alisema bi Mwanaidi Magambo
 ambaye ni Mlezi wa Kituo hicho.
Kituo hicho kina watoto wapatao 
105 ambapo 60 kati yao ni wasichana na 45 wavulana. Kituo hicho kinalea 
watoto wadogo kabisa wa umri wa mwezi mmoja hadi miaka 18. Hivi karibuni
 tulimpokea mtoto mwenye umri wa siku 5 kutoka hospitali ya wilaya ya 
Temeke ambaye mama yake alifariki mara tu baada ya kujifungua, alisema 
bi. Magambo.
Kituo hicho kwa sasa kina matatizo
 ya vyakula, vitanda, magodoro, madaftari pamoja na sare za shule kwa 
ajili ya watoto hao yatima. Bi Magambo alimshukuru sana Mfadhili huyo 
kutoka nchi ya Qatar kwa kuwajengea jengo hilo, lakini alisema kwa sasa 
watahitaji mfadhili wa kuwalipia bili za umeme na maji pamoja na 
mahitaji mengine kituoni hapo.
Kituo hicho kina bahati ya 
kutembelea na warembo wa Miss Tanzania ambapo mwaka 2007, Miss Tanzania 
2000 Jacqueline Ntuyabariwe alitembelea kituo hicho wakati bado wapo 
eneo la Magomeni Makuti na kuwapatia misaada mbalimbali.
Miss Tanzania 201   4 Lilian 
Kamazima alikabidhi vyakula vya aina mbalimbali ikiwemo mchele, unga wa 
ngano, sembe, sukari, maharage, mafuta ya kupikia, sabuni, soda, juisi, 
maji ya kunywa, na biskut vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 
mbili.
Miss Tanzania 2014 Lilian 
aliishukuru kampuni ya Swissport Tanzania ambao ndio waliofadhili ziara 
yake hiyo, na kuwaomba watanzania wengine kujitokeza kwa wingi kusaidia 
watoto yatima na wengine wanaoishi katika mazingira magumu.
Ziara hiyo ya mrembo wa Taifa 
Lilian ilikuwa ni zawadi ya sikukuu za mwisho wa mwaka ambao ililenga 
kuwafariji watoto waliopoteza wazazi wao kwa namna moja au nyingine, na 
pia kutimiza Kauli mbiu ya mashindano ya urembo ya Miss Tanzania isemayo
 [Beauty with Purpose] Urembo na Malengo.



No comments:
Post a Comment