TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, December 28, 2014

WAKAZI WA MKOA WA LINDI WATAKIWA KUSHIKAMANA NA KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KUJILETEA MAENDELEO – MAMA SALMA KIKWETE

IMG_7814Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya Chama Cha Mapinduzi Mama Salma Kikwete akiwahutubia wananchi wa Kata ya Rasibura katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Tawi la Stendi huko Lindi Mjini tarehe 27.12.2014.
 PICHA NA JOHN  LUKUWI     
IMG_7579Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM anayewakilisha Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akizungumza na viongozi wa Tawi la CCM la Mbanja. Mama Salma alitembelea tawi hilo tarehe 27.12.2014 kwa ajili ya kukagua kazi ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi. IMG_7630 Baadhi ya wajumbe wa Tawi la Chama Cha Mapinduzi Mabano katika Kata ya Mbanja wakifurahia hotuba ya Mjumbe wa NEC Taifa wa Lindi Mjini Mama Salma Kikwete wakati alipotembelea Tawi hilo tarehe 27.12.2014. IMG_7656Katibu wa Shina la Wakereketwa Zahanati Kempu Ndugu Hidaya Chivi Ali akikabidhi risala ya wanachama wa Shina hilo kwa Mjumbe wa NEC Taifa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete tarehe 27.12.2014. IMG_7681Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya Chama cha Mapinduzi anayewakilisha Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akiongea na vijana na wananchi mara baada ya kuzindua rasmi shina la wakereketwa Zahanati Kempu lililoko katika Kata ya Rasibura tarehe 27.12.2014.
………………………………………………………………………………
Na Anna Nkinda – Maelezo, Lindi
 Wakazi wa mkoa wa Lindi wametakiwa kushikamana kwa  pamoja, kufanya kazi kwa bidii  na kuzitumia rasilimali zilizopo ili kujiletea maendeleo.
Rai hiyo imetolewa jana Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia wilaya ya Lindi mjini Mama Salma Kikwete wakati akiongea kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mitwero Stendi Kata ya Rasibura wilayani humo.
Mama Kikwete ambaye ni Mke wa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alisema mkoa wa Lindi  umejaliwa kuwa na rasilimali nyingi  ikiwa ni pamoja na zao la korosho, ardhi yenye rutuba, bahari  na  gesi lakini bado kuna changamoto zinazowakabili wananchi na hivyo kukwamisha maendeleo yao.
Alizitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na elimu kwani baadhi ya wanafunzi wafikapo darasa la tano wanaacha  shule kwa ajili ya utoro, mimba za utotoni na vijana kutokufanya kazi kwa bidii.
“Kuna baadhi ya watoto wakifika darasa la tano wanaanza tabia ya utoro hakikisheni wanakwenda shule kusoma kwani elimu itawasaidia katika maisha yao,  msikubali waache shule.  Kutokana na umri wao mdogo wanaona  raha kuacha shule na kwenda kucheza lakini wakifika umri wa utu uzima ndiyo watakapoona umuhimu wa elimu”.
Maisha bora kwa kila mtanzania yanawezekana ikiwa kila mtu atapata elimu itakayomsaidia  katika maisha yake, wakati shule za Sekondari za Kata zinajengwa kuna baadhi ya watu walitubeza na kuziita majina ya ajabu ikiwa ni pamoja na shule za Yeboyebo lakini shule hizi zimewasaidia watoto wengi kutoka familia maskini ambao wameweza kupata elimu”, alisema Mama Kikwete.
Kuhusu  tazizo la mimba za utotoni alisema ni hatari kwa maisha ya Mama na mtoto lakini kama kijana atasoma mimba zitaepukika,  jukumu la wananchi ni kuhakikisha watoto wao wanasoma  kwa bidii na kutokubali  kupewa  mimba ambazo zitawakatisha masomo.
Kwa upande wa vijana MNEC huyo aliwahimiza kuangalia  mstakabali wa maisha yao na kutumia muda wao kufanya kazi kwa bidii kwa kufanya hivyo watapata maendeleo kwani hizi sasa kuna baadhi ya vijana wakati wa  asubuhi wanaacha kwenda shamba kulima na kucheza Pool kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata maendeleo.
“Vijana wengine wanatumia  madawa ya kulevya na kuvuta sigara wanajua kwa kufanya hivyo ndiyo ujanja kitendo ambacho siyo ukweli,  bali unaharibu afya yako na kujirudisha nyuma kimaendeleo. Kama wewe kijana unahitaji kuwa na maisha bora ni lazima uachane na vitendo hivyo na kufanya kazi”, alisisitiza.  
Licha ya kufanya mkutano huo wa hadhara  Mama Kikwete pia alifanya vikao na wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM matawi ya Mbanja, Mabano na Mitwero Stendi na kuwataka wajumbe hao kuwapa vijana  nafasi za uongozi pale watakapojitokeza kugombea nafasi hizo.        
Pia aliwahimiza wajumbe hao wakiwemo vijana, wanawake na wanaume kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika hapo mwakani ili kuwe na ushindani wa kutosha ndani ya chama.
Mama Kikwete yupo wilayani humo kwa ajili ya shughuli za kichama na katika mkutano wa hadhara aligawa kadi kwa  wanachama wapya 23 walijiunga na Chama Cha Mapinduzi.

No comments:

Post a Comment