
Waziri
 wa uchukuzi Mh.Dk. Harrison Mwakyembe ameridhia hatua ya mamlaka ya 
udhibiti usafiri wa nchi kavu na majini ( SUMATRA ) ya kuzuia safari za 
meli ya Mv.Victoria katika ziwa victoria, baada ya meli hiyo kugundulika
 na hitilafu mbalimbali zinazoweza kuhatarisha maisha ya abiria.
Dk. Mwakyembe ameridhika na 
hatua hiyo baada ya uongozi wa bandari ya mwanza kumtembeza sehemu 
mbalimbali za meli hiyo kongwe iliyotengenezwa toka mwaka 1960, na 
kujionea jinsi mitambo yake ilivyochakaa kutokana na kufanya safari zake
 kati ya miji ya mwanza na bukoba kupitia bandari ya kemondo ambapo 
amesema serikali haiwezi tena kurudia makosa, yaliyosababisha meli ya 
Mv.Bukoba kuzama na kupinduka mei 21 mwaka 1996 na kusababisha vifo vya 
watu zaidi ya 800.

Awali kaimu meneja wa kampuni 
ya huduma za meli nchini ( MSC ), fabian mayenga amesema kwamba meli 
hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 1200 na tani 200 mizigo, katika 
ukaguzi uliofanywa na SUMATRA imebainika kuwa haiwezi kuendelea kufanya 
safari zake hadi hapo itakapofanyiwa matengenezo makubwa yanayokisiwa 
kugharimu zaidi ya shilingi bilioni mojahuku akisema vifaa kwa ajili ya 
matengenezo hayo vitawasili nchini katika muda wa wiki 12 hadi 15 ili 
meli hiyo ianze kuendelea kuhudumia wananchi.
Akiwa katika uwanja wa ndege wa 
mwanza kukagua mradi mkubwa wa upanuzi na ukarabati wa uwanja huo 
unaofanywa na kampuni ya Beijing Construction Engineering group kwa 
gharama ya shilingi bilioni 105, waziri huyo wa uchukuzi mh. Dk. 
Harrison Mwakyembe amesema serikali inasikitishwa kulipa deni la 
shilingi bilioni 140 ambalo limesababishwa na ufisadi wa baadhi ya 
watumishi wa shirika la ndege nchini ( ATC ), huku akisema serikali 
inaendelea kukaribisha mashirika mengine ya ndege ili kuweka kwenye 
sekta ya usafiri wa anga.
No comments:
Post a Comment