TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, December 28, 2014

SUMATRA YAIZAMISHA MELI YA MV. VICTORIA-MWAKYEMBE ARIDHIA HATUA HIZO.

Waziri wa uchukuzi Mh.Dk. Harrison Mwakyembe ameridhia hatua ya mamlaka ya udhibiti usafiri wa nchi kavu na majini ( SUMATRA ) ya kuzuia safari za meli ya Mv.Victoria katika ziwa victoria, baada ya meli hiyo kugundulika na hitilafu mbalimbali zinazoweza kuhatarisha maisha ya abiria.

Dk. Mwakyembe ameridhika na hatua hiyo baada ya uongozi wa bandari ya mwanza kumtembeza sehemu mbalimbali za meli hiyo kongwe iliyotengenezwa toka mwaka 1960, na kujionea jinsi mitambo yake ilivyochakaa kutokana na kufanya safari zake kati ya miji ya mwanza na bukoba kupitia bandari ya kemondo ambapo amesema serikali haiwezi tena kurudia makosa, yaliyosababisha meli ya Mv.Bukoba kuzama na kupinduka mei 21 mwaka 1996 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 800.
Awali kaimu meneja wa kampuni ya huduma za meli nchini ( MSC ), fabian mayenga amesema kwamba meli hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 1200 na tani 200 mizigo, katika ukaguzi uliofanywa na SUMATRA imebainika kuwa haiwezi kuendelea kufanya safari zake hadi hapo itakapofanyiwa matengenezo makubwa yanayokisiwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni mojahuku akisema vifaa kwa ajili ya matengenezo hayo vitawasili nchini katika muda wa wiki 12 hadi 15 ili meli hiyo ianze kuendelea kuhudumia wananchi.

Akiwa katika uwanja wa ndege wa mwanza kukagua mradi mkubwa wa upanuzi na ukarabati wa uwanja huo unaofanywa na kampuni ya Beijing Construction Engineering group kwa gharama ya shilingi bilioni 105, waziri huyo wa uchukuzi mh. Dk. Harrison Mwakyembe amesema serikali inasikitishwa kulipa deni la shilingi bilioni 140 ambalo limesababishwa na ufisadi wa baadhi ya watumishi wa shirika la ndege nchini ( ATC ), huku akisema serikali inaendelea kukaribisha mashirika mengine ya ndege ili kuweka kwenye sekta ya usafiri wa anga.

No comments:

Post a Comment