BENDI MPYA•Vijana Ngwasuma 
ilizinduliwa ndani ya Letasi Lounge (zamani Business Park ,Victoria) 
Ijumaa ya tarehe 07-Mar-2014.•Yamoto Band yazinduliwa rasmi tarehe 
21-Sep-2014 ndani ya ukumbi wa Dar Live Mbagala.•Utalii Band yazinduliwa
 Ijumaa ya tarehe 26-Sep-2014 ndani ya ukumbi wa MRC (Mikocheni Resort 
Centre) •Kundi la Chuchu Sound liliibuka tena na kupiga show kadhaa 
katika ukumbi wa Max Bar Ilala. Baadaye kwa sababu kadhaa bendi 
ikapotea.•Pia kulikuwa na bendi ambazo sio mpya lakini ndani ya mwaka 
2014 ziliundwa upya. Bendi hizi ni Victoria Sound  na Ruvu Stars.•Bendi 
nyingine zilizoanzishwa ndani ya mwaka 2014 ni JJ Band, bendi dada ya 
Skylight Band itakayokuwa inatumbuiza mjini Mwanza katika hotel ya Jembe
 ni Jembe. Pia kuna Ruby Band. Bendi hizi 2 zinatarajiwa kuzinduliwa 
rasmi mwanzoni mwa mwaka 2015. UZINDUZI WA ALBUM MPYA•Extra Bongo 
walizindua album ya “Mtenda Akitendewa” Jumamosi ya tarehe 22-Feb-2014 
ndani ya Dar Live Mbagala.•Talent Band (ya Hussein Jumbe) wazindua album
 ya “Kiapo Mara Tatu” Jumatano ya 30-Apr-2014 ndani ya Kisuma Night Pub,
 Temeke (zamani Sugar Ray)•Christrian Bella azindua album ya “Nani Kama 
Mama” ndani ya Mzalendo Pub Jumamosi ya tarehe 30-Aug-2014•Tarsis Masela
 katika viunga vya Ten Lounge (Business Park) Victoria azindua album ya 
“Acha Hizo” Ijumaa ya tarehe 21-Nov-2014•Mashujaa Band yazindua album ya
 “Ushamba Mzigo” kwenye ziara za mikoani. KILI MUSIC AWARD•Kili Music 
Award 2014 ilifanyika Jumamosi ya tarehe 03-May-2014 katika ukumbi wa 
Mlimani City. Kulikuwa na jumla ya vipengele (categories) 8  vya muziki 
wa dansi. Washindi walikuwa kama ifuatavyo;
 1. Mwimbaji Bora wa Kiume-Jose Mara (Mapacha Watatu)
 2. Mwimbaji Bora wa Kike-Luiza Mbutu (Twanga Pepeta)
 3. Rapa Bora-Fergusson (Mashujaa Band)
 4. Wimbo Bora-Ushamba Mzigo (Mashujaa Band)
 5. Bendi Bora-Mashujaa Band
 6. Mtunzi Bora-Christian Bella (Malaika Music Band)
 7. Producer Bora-Amorosso
 8. Hall of Fame (Individual)-Hassan Rehani Bitchuka (Mlimani 
Park Orchestra) WANAMUZIKI WALIOFARIKI•Mpiga tumba wa Twanga Pepeta Soud
 Mohamed “MCD” afariki dunia Jumatatu ya tarehe 27-Jan-2014•Mpiga bass 
wa Vijana Jazz, Maulid Mwangia afariki Jumatano tarehe 12-Mar-2014 na 
kuzikwa Alhamis tarehe 13-Mar-2014•Mwanamuziki mkongwe Muhiddin Gurumo 
afariki dunia Jumapili ya tarehe 13-Apr-2014 na kuzikwa kijijini kwao 
Masaki, Kisarawe Jumanne ya tarehe 15-Apr-2014•Mpiga gitaa wa Skylight 
Band,Chili Challa wa Skylight Band afariki dunia tarehe 
17-Apr-2014.•Amina Ngaluma “Japanese” afariki tarehe 15-May-2014 akiwa 
mji wa Phuket, Thailand.•Mwanamuziki DIGITAL wa FM Academia afariki 
Ijumaa tarehe 18-Jul-2014.•Ally Rashid “Mwana Zanzibar” ambaye mara ya 
mwisho alikuwa mpuliza sax wa Msondo Ngoma afariki tarehe 
10-Oct-2014.•Suzuki Sauti ya Malaika aliyepigia Extra Bongo katika album
 ya “Mjini Mipango” alifariki tarehe 15-Oct-2014•Mwanamuziki Khamis 
Kayumba “Amigoulaus” afariki tarehe 09-Nov-2014.•Mwanamuziki Shem 
Ibrahim Kalenga afariki dunia 15-Dec-2014 na kuzikwa tarehe 16-Dec-2014 
katika makaburi ya Kisutu.•Mnenguaji Aisha Madinda afariki dunia tarehe 
17-Dec-2014 na kuzikwa tarehe 19-Dec-2014. MATUKIO MENGINE 
MAKUBWA•Mdahalo wa kwanza wa aina yake wa kujadili muziki wa dansi 
wafanyika katika ofisi za TBC Jumamosi ya tarehe 05-Apr-2014 chini ya 
u-moderator wa Dacota Khamis, kuhudhuriwa na wadau karibia 30 na 
kuonyeshwa live na TBC2 na baadaye kuonyeshwa recorded na TBC1 kwenye 
kipindi cha “Nyumbani ni Nyumbani”•Bendi ya Msondo Ngoma yafanya sherehe
 za maadhimisho ya kutimiza miaka 50. Maadhimisho yalianza Ijumaa ya 
tarehe 10-Oct-2014 ndani ya Leaders Club na kuhitimishwa TCC Chang’ombe 
Jumamosi ya tarehe 01-Nov-2014. Pia wanamuziki wa bendi walikutana na 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, Alhamis ya
 tarehe 30-Oct-2014. •Kwa mara ya kwanza tukio la “Usiku wa Msanii” 
lafanyika tarehe 25-Oct-2014 katika ukumbi wa Mlimani City. Marehemu 
Father Kanuti alipewa tuzo ya Humanitarian Award.•Tarehe 09-Dec-2014, 
siku ya maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru na miaka 52 ya Jamhuri ya 
Tanganyika (Tanzania Bara), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
Jakaya Mrisho Kikwete katika hafla maalum iliyofanyika katika viwanja 
vya ikulu atoa nishani maalum kwa kundi zima la Atomic Jazz Band ya 
Tanga. Tuzo hiyo ni ya miaka 50 ya Muungano ya daraja la nne. Aliyepokea
 kwa niaba ya kundi ni mzee Stephen Hiza (Mgosingwa). Atomic Jazz Band 
imepewa nishani hiyo kutokana na kazi yao kubwa katika kulihamasisha 
taifa kuenzi muungano hususan kwa kupitia wimbo wao wa “Tanzania 
Yetu”.•Mpambano wa Msondo na Sikinde wafanyika mara mbili kwa kuandaliwa
 na Fred Ogot na kampuni yake ya Bob Entertainment. Mara ya kwanza 
ulifanyika siku ya sikukuu ya Eid Mosi (Eid al-Fitr) tarehe 25-Jul-2014 
ndani ya TCC Chang’ombe. Mara ya pili umefanyika pia TCC Chang’ombe 
Christmas tarehe 25-Dec-2014. Kwenye mpambano wa mara ya pili, kwa mara 
ya kwanza tukio limesindikizwa na bendi ya Vijana Jazz Pambamoto “Saga 
Rumba”.•MAONYESHO YA PAMOJA: Bendi 3 za FM Academia, Mapacha Watatu na 
Ruby Band zapiga pamoja Ijumaa ya tarehe 19-Dec-2014 ndani ya Mzalendo 
Pub. Yamoto Band mara kadhaa imefanya maonyesho ya pamoja kwa kupiga 
pamoja na Mapacha Watatu, Skylight Band na Twanga Pepeta. Pia Mlimani 
Park Orchestra wamepiga pamoja mara kadhaa na Machozi Band ya Lady 
Jaydee. Ruby Band walipiga pamoja na Twanga Pepeta Jumapili ya tarehe 
28-Dec-2014 ndani ya Leaders Club•Onyesho la Miaka 16 ya Luizer Mbutu 
ndani ya Twanga Pepeta lililokuwa lifanyike Jumamosi ya tarehe 
20-Dec-2014 limeahirishwa hadi tarehe 31-Jan-2015 kutokana na kifo cha 
mnenguaji Aisha Madinda.•Mechi ya mpira wa miguu kati ya kundi la BONGO 
DANSI na kundi la WATANASHATI WA MUJINI lafanyika katika viwanja vya 
Leaders Club Jumapili ya tarehe 23-Nov-2014. Matokeo yalikuwa suluhu 
0-0. Kundi la BONGO DANSI mara kadhaa limefanya ziara ya kumtembelea 
Nguza Vicking na Papii Kocha ambao wapo gerezani Ukonga. •Tarehe 
26-Dec-2014, umoja wa wanamuziki wa dansi katika viwanja vya Karimjee 
wafanya dua maalum ya kumuombea Rais Jakaya Kikwete ili hali yake ya 
kiafya iimarike.

No comments:
Post a Comment