Mkurugenzi
 wa Mboni Show, Mboni Masimba (wa pili ktoka kulia) akizungumza na 
waandishi wa habari jana katika  ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo 
jijini Dar es Salaam wakati akitangaza kuanza kwa msimu wa tatu wa 
kipindi chake ‘The Mboni Show’ kinachotarajia kuanza Jan 2, 2015. 
Kushoto ni kiti Simpompa na kuanzia kulia ni Afisa Masoko wa Mfuko wa 
Taifa wa Hifadhi ya Jamii (PSPF) Magira Werema na Kaimu Mkurugenzi wa 
Masoko TBC,Bw.Fadhili Chilumba.
Kutoka
 Kulia Afisa Masoko wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (PSPF) Magira 
Werema akizungumza wakati wa uzinduzi kipindi cha Mboni Show uliofanyika
 katika Ukumbi wa Idara Habari Maelezo jijini Dar es Salaam. Pembeni ni 
Kaimu Mkurugenzi wa Masoko TBC,Bw.Fadhili Chilumba pamoja na Mkurugenzi 
wa Mboni Show, Mboni Masimba.
Na Mwandishi Wetu.
Mkurugenzi
 wa Mboni Show, Mboni Masimba ameamua kuhamishia kipindi cha Mboni show 
katika kituo cha utangazaji cha Taifa (TBC) kutoka EATV ili kuvutia 
watazamaji wengi na wapya kwa wazee pamoja na vijana.
Kipindi cha Mboni Show kitaanza kurushwa TBC kuanzia January 2 mwaka 2015 siku ya
Ijumaa saa 3 Usiku-4 Usiku na marudio Jumanne saa 9:00 mchana-10:00mchana.
Akizungumza
 na waandishi wa habari jana jijini Dar ndani ya ukumbi wa Idara ya 
Habari (MAELEZO), Mboni Masimba ametoa shukrani kwa EATV kwa ushirikiano
 wao kwa kipindi chote alichokuwa nao,na kusema kuwa amehamishia kipindi
 cha Mboni Show katika kituo cha TBC ili kuvutia watazamaji wengi hakuna
 atakaye tumia jina la Mboni Show na hakuna kitakachomkwamisha kwa vile 
ana hati miliki.
“Nimeamia
 TBC kwa kuwa nahitaji watazamaji wengi ,wote wazee na vijana na hakuna 
atakaye tumia jina langu la Mboni Show kwa kuwa nina hati miliki ya jina
 hili”alisema Mboni.
Kwa
 upande wake,Kaimu Mkurugenzi wa Masoko TBC, Bw.Fadhili Chilumba amesema
 wamefurahi kuwepo kwa Mboni Show katika kituo cha Taifa(TBC) na kutoa 
wito kwa mashabiki kuweza kuwadhamini watu kama wakina Mboni na 
wanamkaribisha sana.
Nao
 wadhamini wa Mboni Show,Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (PSPF) 
Magira Werema wamesema wanamwezesha Mboni kuwepo hewani ili 
kuhamasisha,kuelimisha pamoja na kuburudisha umma wa Watanzania.


No comments:
Post a Comment