Maafisa
 nchini Somali wanasema kuwa kiongozi mkuu wa kundi la wapiganaji wa 
Alshabaab amekamatwa karibu na mji mmoja karibu na mpaka wa Kenya na 
Somali.
Kamishna wa Wilaya ya El Wak mjini Gedo ameiambia BBC 
Somalia kwamba vikosi vya usalama vilimkamata Zakariya Ismail Ahmed 
Hersi katika maficho yake ndani ya nyumba moja baada ya kupashwa habari.
Mwaka 2012 Marekani ilitoa zawadi ya dola millioni 3 kwa yeyote yule ambaye angeweza kutoa habari za Hersi.
Kundi
 la Al Shabaab limejiondoa kutoka miji kadhaa nchini Somalia tangu 
uzinduzi wa mashambulizi makali dhidi ya kundi hilo yanayotekelezwa na 
vikosi vya AMISOM vikishirikiana na wanajeshi wa serikali ya Somalia.
Bwana Hersi alikuwa kiongozi wa kundi la Alshabaab upande wa Amniyat.
Mapema
 mwaka huu alikosana na kiongozi wa kundi hilo Ahmed Abdi Godane ambaye 
aliuawa katika mashambulizi ya Marekani mnamo mwezi Septemba.

No comments:
Post a Comment