AZAM, MTIBWA, SIMBA, YANGA KUCHEZA MAPINDUZI
Timu za Azam, Mtibwa Sugar, Simba 
na Yanga zitashiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi inayofanyika 
kisiwani Zanzibar kuanzia Januari 1 hadi 13 mwakani.
Shirikisho la Mpira wa Miguu 
Tanzania (TFF) limetoa ruhusa kwa timu hizo kucheza mashindano hayo 
baada ya kuhakikishiwa na Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kuwa 
kesi iliyofunguliwa dhidi ya viongozi wake imeondolewa mahakamani.
Kutokana na timu hizo kushiriki 
Kombe la Mapinduzi, mechi zao za raundi ya tisa na kumi ya Ligi Kuu ya 
Vodacom (VPL) zitachezwa katikati ya wiki baada ya kumaliza mechi zao za
 michuano hiyo.
Hivyo mechi za VPL ambazo 
hazitachezwa wikiendi hii ni kati ya Azam na Mtibwa Sugar, Mbeya City na
 Yanga, na ile kati ya Mgambo Shooting na Simba. Mechi za wikiendi ijayo
 zinazopisha michuano hiyo ni kati ya Kagera Sugar na Azam, Coastal 
Union na Yanga, Mbeya City na Simba, na Mtibwa Sugar na Tanzania 
Prisons.
18 WAPATA BEJI ZA UAMUZI FIFA
Waamuzi 18 wa Tanzania wamepata beji za uamuzi za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kwa mwaka 2015.
Idadi hiyo ambayo ni rekodi kwa 
Tanzania inahusisha waamuzi saba wa kike. Waamuzi wa kati wa kike 
waliopata beji hizo ni pamoja na Jonesia Rukyaa Kabakama aliyechezesha 
mechi ya Nani Mtani Jembe kati ya Simba na Yanga. Wengine ni Florentina 
Zablon Chief na Sophia Ismail Mtongori.
Waamuzi wasaidizi wa kike 
waliopata beji hizo ni Dalila Jafari Mtwana, Grace Wamala, Hellen Joseph
 Mduma na Kudura Omary Maurice.
Kwa waamuzi wa kati wa kiume ni 
Israel Mujuni Nkongo, Martin Eliphas Sanya, Mfaume Ali Nassoro na Waziri
 Sheha Waziri. Waamuzi wasaidizi ni Alli Kinduli, Ferdinand Chacha, 
Frank John Komba, John Longino Kanyenye, Josephat Deu Bulali, Samuel 
Hudsin Mpenzu na Soud Iddi Lila.

No comments:
Post a Comment