TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, January 10, 2015

shilole apagawisha vilivyo Mabibo hosteli kwenye hafla ya UNI255- COLLEGE CHAMPIONSHIP DAR ES SALAAM.

 
 
 
 
 
 
 
Fainali ya Michuano ya Michezo kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, imeshereheshwa na burudani kabambe kutoka kwa wasanii mbali mbali wa muziki, lakini pia burudani kubwa ilikuwa ni kwa wanafunzi walioonyesha vipaji vyao kutokana na kuwa na khari wakti wote wa kujieleza, kujibu maswali ambapo wanafunzi mbali mbali wameweza kujipatia zawadi kutoka Kampuni ya Simu za Mkononi Airtel Tanzania, ambao ndiyo Wadhamini Wakuu walioweza kufanikisha Shughuli hiyo, ambayo kwa Wanafunzi hao pia ilikuwa ni kupata Timu za College zitakazoshiriki Ligi ya Dar es Salaam inayoshirikisha pia Vyuo vya Pwani na Bagamoyo, Michuano ya Kutafuta Timu za Vyuo ni Mpango unaoratibiwa na Kampuni ya Miss Demokrasia Tanzania, iliyopewa dhima na wenye haki Miliki ya kuwa waamdaji wa Michezo hiyo Kila Mwaka.
Vyuo ambavyo Tayari vimefanikiwa kuingia kwenye kinyang'anyiro hicho cha NACTE INTER COLLEGE  Championship Mpaka sasa baada ya kushinda Michezo yake kwenye Makundi kwa njia ya Mtoano, iliyofanyika kwenye viwanja mbali mbali vya  vyuo ikiwemo D.I.T, Shirika la Elimu Kibaha, Ustawi wa Jamiii, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Viwanja vya Mabibo Hosteli, N.I.T na Bandari College, Wenyeji wameweza kuingia hatua ya pili pamoja na timu za I.F.M, CBE, TRA,MUHIMBILI, COET,COSS,UDBS.

Wengine ni Mwalimu Nyerere Memorial Academy,Institute of Adult Education, Kilimanjaro Institute College, St. Joseph  College, Zoom Polytechnic College , Tanzania Institute of Accountancy (TIA,Njuweni Institute of Hotel, Catering & Tourism Management, Bagamoyo College of Arts (TaSUBa), St. Mary Teachers College, na  Dar es salaam City College (DACICO).
 
 Zaidi ya Vyuo mia nne 400 vilivyopata usjali wa NACTE Tanzania vilitakiwa kushiriki michezo hiyo lakini kutokana na sababu mbali zilizowasilishwa na vyuo baadhi yao hawataweza kushiki kwa mwaka huu kutokana na kile walichosema Maandalizi ya kustukiza ambapo  wamewataka waandaaji kutoa taarifa mapema ili kila chuo kiweze kuwaandaa wachezaji kwa ajili ya kushiriki huku vyuo vingine vikiwa havina wachezaji wa kuweza kushiriki.

 Ratiba ya Michuano hiyo inaanza April ambapo timu hizo zitacheza ligi ya Nyumbani na Ugenini na itachuku siku 45 hadi kumalizika zikiwa ni siku za wikiend kuanzia April mosi hadi Mey 24, sambamba na Vyuo vya Mikoa ya Kanda ya Ziwa, kanda ya Kaskazini, kanda ya  Kati, Kanda ya Kusini, na Kanda ya Zanzibar zitashiriki Michuano hiyo na timu zitakazofanikiwa kuibuka na Ubingwa kwa kila kanda zitakutana kutafuta Bingwa wa chuo bora katika michezo Tanzania(NACTE) (The best in sports college Tanzania).
(Picha na Mpiga Picha wa MIDETA Entertainment)


 

No comments:

Post a Comment