TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 6, 2015

MATUKIO YA PICHA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI KITUO CHA POLISI MBWENI ZANZIBAR.

unnamed1aNaibu Waziri wa Ardhi Makaazi Maji na Nishati Haji Mwadini Makame akifungua kitambaa kuashiria Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Kituo cha Polisi mbweni nje ya mji wa Zanzibar ikiwa ni Shamra shamra za kutimia miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar. unnamed2a-Vijana wadogo kutoka katika kituo cha Nyerere Shaolin Group wakionyesha umahiri wa kuweza kupambana na uhalifu katika sherehe za Uwekaji wa jiwe la Msingi la Kituo cha Polisi mbweni nje ya mji wa Zanzibar ikiwa ni Shamra shamra za kutimia miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar. unnamed3aKamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Omar akitoa maelezo kuhusiana na Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Kituo cha Polisi mbweni nje ya mji wa Zanzibar ikiwa ni Shamra shamra za kutimia miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar. unnamed4a-Katibu Mkuu Wizara ya mambo yandani Mbaraka Abdullwakili akitoa hotuba na kumkaribisha mgeni rasmi katika Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Kituo cha Polisi mbweni nje ya mji wa Zanzibar ikiwa ni Shamra shamra za kutimia miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar. unnamed5a-Naibu Waziri wa Ardhi Makaazi Maji na Nishati Haji Mwadini Makame akitoa hotuba katika Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Kituo cha Polisi mbweni nje ya mji wa Zanzibar ikiwa ni Shamra shamra za kutimia miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar.kushoto yake ni Katibu Mkuu Wizara ya mambo yandani Mbaraka Abdullwakili na kulia ni Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Omar. unnamed6aNaibu Waziri wa Ardhi Makaazi Maji na Nishati Haji Mwadini Makame katikati akiwa katika Picha ya pamoja na Viongozi wa Jeshi la Polisi katika Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Kituo cha Polisi mbweni nje ya mji wa Zanzibar ikiwa ni Shamra shamra za kutimia miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.
…………………………………………………….
Na Ali Issa Maelezo-Zanzibar. 5/1215
Katika kufanikisha kuwafichua na  kuwakamata wahalifu wa vitendo viovu  vya ujambazi na ubakaji kunahitaji ushirikiano mkubwa kati ya Jeshi la Polisi na wananchi wanaoishi katika maeneo yao.
Hayo yamesemwa leo huko Mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar na Naibu Waziri wa Aridhi, Makazi, Maji na Nishati Haji Mwadini Makame wakati wa uzinduzi wa kituo cha Polisi kijijini hapo.
Amesema Jeshi la Polisi liko tayari kufanya kazi na raia wema  katika maeneo yao kwa kuwafichua wahalifu na kuwatia hatiani kwani wananchi ndio wanaoishi katika maeneo yanayofanyiwa uhalifu na kuwepo uwezekano mkubwa wa kufanikisha kazi zao. 
“Wananchi  shirikianeni kuwafichua  wanaofanya vitendo vya uhalifu,  ujambazi, uvutaji wa bangi na uuzaji wa madawa ya kulevya ili kazi ya  jeshi la polisi  ya kuwatia hatiani iwe rahisi”, alisema Haji Mwadini.
Aidha alisema kuwa kujengwa kituo cha Polisi katika eneo hilo la Mbweni ni faraja kubwa kwa jamii inayoishi hapo kwani lengo kuu ni kuwepo ulizi na usalama wa raia na mali zao hivyo alitaka kituo hicho kutumike kwa maengo yaliyokusudiwa. 
Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame akimkaribisha mgeni rasmi katika hafla hiyo, alisema kuwa kituo hicho kimejengwa kwa msaada wa mdau mzalendo ili kuwanusuru wananchi wanaoishi maeneo hayo na vitendo viovu vya ujambazi na uhalifu.
Aliwaomba wananchi wanaoishi wa hapo  kukitumia kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi  kuanzisha ulizi shirikishi.
Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani Mbaraka Abdul Wakili alisema kuwa Jeshi la Polisi limekuwa na changamoto nyingi za kupambana na vitendo vya ujambazi, hata hivyo wameweza kufanikiwa kuwadhibiti majaambazi.
Alisema  kujengwa kwa kituo hicho ni mfululizo wa kujenga vituo vyengine kwa daraja A na C katika maeneo ya Pongwe, Mbuyutende na Jozani kwa Unguja.
Ameongeza kuwa wamekuwa wakijenga vituo  pembezoni mwa fukwe za Bahari ili  kwanusuru watalii na wananchi  wa maeneo hayo kwa kuwapa ulizi  wa uhakika.
Uzinduzi wa kituo cha Polisi Mbweni ni moja ya shamrashamra za maadhimisho ya  miaka 51 ya Mapinduzi matukufu  ya Zanzibar ya 1964.  

No comments:

Post a Comment