Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (mwenye 
koti la suti) akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa Pemba kwa ajili 
kuhuduria sherehe za uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani jimbo la Mkanyageni,
 Kusini Pemba na kupokelewa na Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na 
Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) 
Bw. Al Amin Yusuph (kulia) aliyeambatana na Mshauri na Mkufunzi kutoka 
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. 
Rose Haji Mwalimu (aliyeongoza mbele).
Na Mwandishi wetu, Pemba
SERIKALI
 ya Mapinduzi Zanzibar imesema kwamba itaendelea kuruhusu kuanzishwa kwa
 Redio za jamii kutokana na umuhimu wake katika kuhimiza maendeleo na 
kutumika kama daraja kati ya wananchi na serikali yao.
Hayo 
yalisemwa na Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na 
watoto, Zainab Omar Mohammed wakati akizundua kituo cha redio ya jamii 
jimbo la Mkanyageni, Mkoani Pemba.
Shughuli
 hiyo ambayo ilifanyika kama sehemu ya shamra shamra za sherehe za 
mapinduzi kutimiza miaka 51 zilihudhuriwa pia na wafadhili wa mradi huo 
ambao ni Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la Elimu, Sayansi na 
Utamaduni (UNESCO).
Waziri
 huyo alisema kwamba uzinduzi wa kituo cha redio ya jamii katika jimbo 
la Mkanyageni Mkoani Pemba ni moja ya azma ya serikali ya Mapinduzi ya 
Zanzibar kuwapa haki wananchi wake ya kupata habari ikiwa ni sehemu 
muhimu sana ya maisha ya wanadamu.
Munekano wa sehemu ya jengo la Redio Jamii Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini Pemba kabla ya kuzinduliwa rasmi.
Alisema
 habari ni kitu muhimu sana katika maisha ya sasa na wakati taifa 
likiadhimisha miaka 51 ya mapinduzi yaliyolenga kubadili maisha ya 
wazanzibari uwapo wa redio za jamii ni kitu ambacho kitasukuma mbele 
zaidi madhumuni ya mapinduzi , kumkomboa mzanzibari kiuchumi na 
kifikira.
“Redio
 hizi Jamii, zimewekwa na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa 
madhumuni ya kuwapa fursa wananchi kupata habari,kupata burudani, kupata
 elimu, lakini pia kutoa fursa ya kutoa mawazo yao kupitia redio hizi 
ili serikali ipate kujua zaidi nini hasa changamoto za wananchi na iweze
 kuzifanyia kazi kwa urahisi zaidi” alisema Waziri Zainab.
Pamoja
 na kuushukuru Umoja wa mataifa kwa kusaidia redio za jamii aliutaka 
Umoja huo uendelee kuimarisha uwezo wa redio hizo ili wananchi wazitumie
 kupata maendeleo.
Naye 
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez amesema
 Umoja wa mataifa unajisikia fahari kuwezesha asilimia 60 ya wazanzibari
 kusikiliza redio za jamii na kuzitumia katika maendeleo yao.
Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez 
aliyeambatana na mkewe akisalimiana na Ofisa mdhani kutoka Wizara ya 
Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar na Mjumbe wa bodi ya 
usimamizi Redio Jamii Micheweni, Ali Mohamed mara baada ya kuwasili eneo
 la tukio.
Alisema
 umoja huo utaendelea na ushirikiano wake na serikali ya Mapinduzi 
Zanzibar ya kuweka mazingira ya upatikanaji wa habari kuwa bora zaidi, 
ushirikiano ambao waliuanza mwaka 2008 wakati wa kutengeneza sera ya 
utangazaji.
Alisema ni sera hiyo iliyowezesha kuwepo kwa redio za jamii na utangazaji wa umma.
Alisema
 Redio za jamii ni msaada mkubwa katika kutoa elimu kwa jamii 
inayozunguka kituo hicho na kusema kwamba ni imani yake kituo cha Mkoani
 kitafanya kazi iliyokusudiwa kwa kuhamasisha mawazo chanya ya maendeleo
 na kuleta ushirikiano na amani inayotakiwa katika jamii.
Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) na
 Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa 
la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph wakipitia 
ratiba kabla ya kuanza rasmi sherehe za uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani 
uliofanyika Kusini Pemba.
Amesema Umoja wa Mataifa umewezesha kituo hicho vifaa vya utangazaji na kutengeneza uwezo wa wafanyakazi wa chombo hicho.
Amesema
 kupitia mradi wa uwezeshaji demokrasia (EDP) unaoendeshwa kwa pamoja na
 UNESCO na UNDP chini ya makubaliano ya msaada kwa serikali ya Tanzania 
na Umoja wa Mataifa (UNDAP) , Umoja wa Mataifa umetoa mtambo wa kurushia
 matangazo wenye nguvu za Watts 600 unaoweza kusambaza matangazo yake 
eneo lote la Kusini pemba.
 
Pamoja na mtambo huo na vifaa vingine vya studio vilitolewa na 
kumefanyika ufundishaji wa watangazaji namna bora ya mawasiliano na 
menejimenti ya habari na utawala.
Mratibu
 huyo aliitaka serikali na taasisi zake kukitumia vyema kituo hicho 
katika kuhakikisha kwamba maendeleo yaliyokusudiwa kwa jamii 
yanapatikana kupitia vipindi mbalimbali vya kuelimishana.
Mke
 wa Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa 
Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bi. Fainula 
Kurji-Rodriguez (kushoto) na Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja
 wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji 
Mwalimu wakifurahia burudani ya Ngoma ya Msembwe ya Kusini Pemba 
ilipokuwa ikisherehesha kabla ya kuwasili wa mgeni rasmi katika uzinduzi
 huo.
Pia 
aliwataka waendeshaji wa kituo hicho kuwa makini na kuwajibika kwa umma,
 kauli ambayo awali pia ilielezwa na Naibu Katibu Mkuu , Wizara ya 
habari Utamaduni , Utalii na Michezo Juma Yakufi aliyetaka sheria na 
taratibu za mawasiliano kuzingatiwa.
Alitaka
 vipindi vitakavyotengenezwa kuzingatia utu, silka na utamaduni wa 
Mzanzibari na redio hiyo kuendeshwa kwa mujibu wa masharti ya redio 
jamii kwa kuhakikisha hawaingiliwi na taasisi yoyote na kuendeshwa kwa 
manufaa ya jamii na sio manufaa ya mtu mmoja mmoja.
Naye 
Mwa redio hiyo Ali Abbas pamoja na kushukuru kusaidia kuanzishwa kwa 
redio hiyo aliitaka jamii kuitumia vyema nafasi waliyopewa kuendeleza 
mbele maendeleo yao na kutumia upashanaji habari kutanzua changamoto za 
maendeleo.
Mshauri
 na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na 
Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu akijumuika kutoa burudani na 
kikundi cha Ngoma ya Msembwe kutoka Kusini Pemba.
Katibu
 Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Zanzibar (ZBC), Chande Omar (kulia) 
akifafanua jambo kwa Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na 
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) kabla ya kuanza kwa sherehe za 
uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani iliyopo Kusini Pemba. Katikati ni Afisa 
Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la 
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph na kushoto ni 
Mke wa Mratibu Mkazi wa UN Tanzania, Bi. Fainula Kurji-Rodriguez.
Meneja
 wa Redio Jamii Mkoani jimbo la Mkanyageni Mkoani Kusini Pemba, Bw. Ali 
Abbas akisoma risala ya kituo chake mbele ya mgeni rasmi Waziri wa 
Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto visiwani 
Zanzibar, Mh. Zainabu Omari Mohammed (hayupo pichani) wakati wa sherehe 
za uzinduzi wa kituo hicho cha redio.
Mabinti
 wa visiwani Pemba wakisoma utenzi wa kulishukuru shirika la UNESCO na 
ZBC kwa kuanzisha kituo hicho cha Redio jamii jimbo la Mkanyageni mkoani
 Kusini Pemba.
Naibu
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo visiwani 
Zanzibar, Juma Yakufi akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri mwenye dhamani 
ya wizara hiyo wakati wa sherehe za uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani jimbo
 la Mkanyageni mkoani Kusini Pemba uliofanyika mwishoni mwa wiki 
visiwani humo.
Mkuu
 wa Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba, Hemedi Selemani akitoa neno la 
shukrani wakazi wa mkoani jimbo la Mkanyageni pamoja na wageni waalikwa 
kwenye sherehe za uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba 
uliofanyika mwishoni mwa wiki.
Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez 
akizungumza kwenye uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba 
uliofanyika mwishoni mwa wiki.
Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez 
akimkabidhi cheti Meneja wa Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba, Bw. Ali 
Abbas wakati wa sherehe za uzinduzi wa Redio jamii hiyo.
Mkuu
 wa Mkoa wa Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini Pemba, Bi. Mwanajuma 
Abdallah akizungumza machache na wakazi wa mkoani na kuwaasa kukitumia 
chombo hicho vyema katika kujiletea maendeleo na kupashana habari kabla 
ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzindua rasmi kituo hicho cha Redio Jamii.
Waziri
 wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab 
Omar Mohammed akisoma hotuba yake kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo 
cha redio ya jamii jimbo la Mkanyageni, Mkoani Kusini Pemba.
Pichani
 juu na chini ni baadhi ya wakazi wa Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini 
Pemba wakifuatilia kwa umakini hotuba ya mgeni rasmi kwenye sherehe za 
ufunguzi wa kituo hicho cha Redio Jamii.
Pichani
 juu na chini ni Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake
 na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akikabidhi vyeti kwa baadhi ya 
wafanyakazi wa Redio Jamii Mkoani ya jimbo la Mkanyageni mkoani Kusini 
Pemba. Anayeshuhudia tukio hilo ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja 
wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa 
(UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya 
Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo visiwani Zanzibar, Juma Yakufi.
Mgeni
 rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na 
watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi 
wa kituo cha Redio Jamii Mkoani iliyopo Kusini Pemba. Wanaoshuhudia 
tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini Pemba, 
Bi. Mwanajuma Abdallah (mwenye mtandio wa bluu), Mkuu wa Wilaya ya 
Mkoani Kusini Pemba, Hemedi Selemani pamoja na Mratibu Mkazi wa 
mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la 
Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
Mgeni
 rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na 
watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akitia saini kitabu cha wageni cha 
kituo cha Redio Jamii Mkoani Kusini Pemba kabla ya kukagua vifaa na 
studio ya kituo hicho.
Mgeni
 rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na 
watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed akizungumza Live na wananchi wa jimbo 
la Mkanyageni mkoani Kusini Pemba mara baada ya kuzindua kituo cha Redio
 Jamii Mkoani ikiwa ni shamra shamra ya sherehe za Mapinduzi mwishoni 
mwa wiki kisiwani Pemba. Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na washika dau kutoka UNESCO.
Mtangazaji
 wa kituo cha Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba, Bw. Seif Mohammed 
akiwa kwenye mahojiano na Mgeni rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa 
jamii, Vijana, wanawake na watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed yaliyorushwa
 Live na kituo hicho mara baada ya kuzinduliwa.
Mgeni
 rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na 
watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed katika picha ya pamoja na wafanyakazi 
wa Redio Jamii Mkoani, Wajumbe wa Bodi ya Redio Jamii Mkoani, wafadhili 
pamoja na baadhi ya wageni waalikwa.
Mgeni
 rasmi Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa jamii, Vijana, wanawake na 
watoto, Mh. Zainab Omar Mohammed katika picha ya pamoja na wajumbe wa 
bodi ya Redio Jamii Mkoani jimbo la Mkanyageni Kusini Pemba.
Mshauri
 na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na 
Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu akiwa kwenye picha na wanafunzi
 wake wa vituo vya redio jamii ya Mkoani na Micheweni mara baada ya 
sherehe za uzinduzi.
Kikundi
 cha Ngoma ya Msembwe cha kisiwani Pemba kikitoa burudani kwenye 
uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani uliofanyika mwishoni mwa juma Kusini 
Pemba.








No comments:
Post a Comment