TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 6, 2015

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MALUWI WAJISAIDIA MAPORINI

unnamedRIZ1
Na Mwamvua Mwinyi,Bwilingu.

WANAFUNZI wa shule ya msingi Maluwi,Mtambani,kitongoji cha Mdaula,kata ya Bwilingu,jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani,wanakabiliwa na kero ya ukosefu wa vyoo suala linalowasababishia kwenda kujisaidia maporini.
Wakati huo huo walimu na wanafunzi wa shule hiyo wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji na kupelekea kufuata maji mtoni ambako maji yake sio salama kutokana,nyakati za mvua kusomba vinyesi na uchafu mbalimbali unaoingia mtoni humo.
Akizungumzia kero hiyo ,juzi,shuleni hapo,mwalimu mkuu wa shule ya Maluwi,Shabani Makuka alisema changamoto hizo sio za wanafunzi pekee bali hata walimu wanashida ya vyoo kutokana na sasa wanatumia choo kilichojengwa kwa nyasi.
“Shule hii kijumla na wakazi wa Mtambani pia inakumbwa na kero ya ukosefu wa huduma za kiafya hali inayosababishia kufuata huduma za kiafya Chalinze ambako umbali wake ni km zaidi ya 15 kutoka Mtambani,na kwa wale wanaoshindwa kwenda Chalinze uamua kumeza panadol za kununua bila ushauri wa daktari”alisema Mwalimu mkuu huyo.
Aidha Makuka alisema zipo changamoto nyingine ambazo ni pamoja na uhaba wa madarasa,madawati na utoro mkubwa unaofanywa na wanafunzi hasa walio jamii ya wafugaji ambao utoroka na kwenda kuchunga mifugo nyakati za masomo.
Hata hivyo Makuka alisema zipo hatua walizozichukua tangu ahamie kwenye shule hiyo mwaka 2013 ambapo aliwaomba amjirani kuwa wakisaidia wanafunzi hao kujistili pale inapobidi hasa kwa watoto wakike ambao wamepevuka.
Pia walichangisha wananchi na kupata kiasi cha sh.1,200,000 na halmashauri ilitenga fedha na kuwapatia  mil 2.5 jumla mil 3.7 ambazo wanatarajia kujenga choo kitakachosaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa choo shule hapo.
Changamoto hizo zilifikishwa kwa mbunge mwenye dhamana ya kusimamia kero za wananchi jimboni chalinze Ridhiwani Kikwete ambae alisema kitendo cha kujisaidia maporini ni hatari kwa wanafunzi.
Ridhiwani alisema atachukua hatua za haraka kuangalia namna ya kutatua kero zilizopo shuleni hapo kwa kushirikiana na kamati ya shule na halmashauri ya wilaya .
Shule ya msingi Maluwi  imejengwa miaka 10 iliyopita,ina jumla ya wanafunzi 203,upungufu wa madawati 35 yaliyopo 45.

No comments:

Post a Comment