Kaimu
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anna Rose Nyamubi (mbele) akizungumza na 
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) pamoja na 
watendaji wake waliomtembelea ofisini kwake kabla ya kuanza ziara rasmi 
katika mkoa wa Shinyanga. Profesa Muhongo anafanya ziara katika mkoa huo
 kukagua miradi ya umeme inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini 
(REA) Awamu ya Pili pamoja na kuzungumza na wananchi.
Waziri
 wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisalimiana na baadhi ya
 wakazi wa wilaya ya Kishapu mara baada ya kuwasili wilayani humo. 
Kushoto ni Mbunge wa Kishapu Suleiman Masoud Nchambi
Wakazi
 wa Kata ya Bubiki wilayani Kishapu wakimpokea kwa shangwe Waziri wa 
Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo mara alipowasili wilayani 
hapo huku wakiwa na mabango yaliyosomeka “ Profesa wa Kweli, Nchi sasa 
inang’aa vijijini, Wewe ni Jembe”.
Mmoja
 wa wakinamama kutoka kata ya Igubi wilayani Kishapu mkoani Shinyanga 
akimfunga vitambaa mkononi Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter 
Muhongo kama heshima kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kusambaza umeme 
katika kata hiyo. Kata hiyo ni moja ya kata zinazonufaika na mradi wa 
umeme vijijini unaotekelezwa na REA Awamu ya Pili
Mbunge
 wa Kishapu Suleiman Masoud Nchambi (katikati) akijumuika na wakazi wa 
Kata ya Igumbi iliyopo wilayani Kishapu kucheza ngoma ya kumpongeza 
Waziri wa Nishati na Madini kwa juhudi zake za kusambaza umeme katika 
kata hiyo pamoja na jimbo lake.
Waziri
 wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) na Mbunge wa 
Kishapu Suleiman Masoud Nchambi (kulia) wakifuatilia taarifa ya 
utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini inayosimamiwa na REA Awamu ya 
Pili iliyokuwa inatolewa na Meneja Utaalamu Elekezi kutoka REA Gissima 
Nyamohanga (hayupo pichani)
Mtaalamu
 kutoka kampuni ya kusambaza umeme vijijini ya LTL (PVT) LTD Michael 
Marenye (kushoto) akitoa taarifa ya hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa 
miundombinu ya umeme katika wilaya ya KIshapu. Kulia ni Waziri wa 
Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Waziri
 wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisisitiza jambo 
alipokuwa akizungumza na wakazi wa Kata ya Mwamalasa wilayani Kishapu.
Mbunge wa Jimbo la Kishapu Suleiman Masoud Nchambi akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo
Wakazi
 wa Bubiki wilayani Kishapu wakimkabidhi Waziri wa Nishati na Madini 
Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) zawadi ya mbuzi wawili kama pongezi 
kwa kazi nzuri ya kusambaza umeme katika kata hiyo. 
Sehemu
 ya umati wa watu kutoka Kata ya Bubiki wakishangilia hotuba ya Waziri 
wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani).


No comments:
Post a Comment