Meneja uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando
……………………………………………………………………………….
Kampuni ya simu za mkononi ya 
Airtel leo imebainisha kuwa mwishoni mwa wiki hii itazindua rasmi huduma
 mpya maalum kwaajili ya kutoa huduma nafuu za mawasiliano kwa wanafunzi
 walioko vyuoni katika chuo kikuu cha Dar es salaam UDSM ambapo hafla ya
 uzinduzi wa huduma hiyo inayojulikana kama Airtel UNI 255 kwa vyuo 
vikuu vilivyopo Dar es salaam itafanyika katika viwanja vya Mabibo 
hostel  
Akiongea kuhusiana na uzinduzi wa 
huduma hiyo Meneja uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando amesema 
“Airtel Uni 255 ni huduma pekee yakibunifu toka Airtel Maalum kwa 
wanafunzi wa vyuo yenye kuwapa unafuu wa kuwasiliana wawapo chuoni, sasa
 wanafunzi wote wa chuo wanapotaka kupata nyongeza ya vile wanavyosoma 
kwenye mtandao huduma  hiii  ndio jibu sahihi kwao kutokana na unafuu 
wake kwenye inteneti, kupiga simu na hata sms. Huduma hii tayari 
tumeshaizindua kwa vyuo vikuu vingine vya Dodoma, Mbeya, Iringa, Mwanza 
na imeonyesha mafanikio makubwa sana kwa watumiaji wakiwemo wanafunzi na
 wale wote wanaotumia huduma hii maeneo ya vyuo”
“Airtel tumeona ni vyema tuizindua
 hapa katika vyuo vya Dar es salaam wiki hii siku ya Jumamosi pale 
mabibo hostel ambapo mbali na uzinduzi kutakuwa na tamasha kubwa 
litakalopambwa na watoa burudani nguli akiwemo Ney wa Mitego, Roma 
Mkatoliki, Shilole pmaoja na DJ maarufu jiji Dj Zero aliongeza kusema 
Mmbando 
Nae meneja wa huduma hiyo ya UNI 
255 Anethy Muga alisema “Airtel tumeoana hii ni huduma maalum kwa 
wanafunzi na ndio maana tukaona ni vyema kuizindulia katika Hostel zao 
pale mabibo ambapo tunaamini wanafunzi wengi wa chuo kikuu hapa jijini 
wanaifahamu na wanaishi mabibo hivyo wanakaribishwa katika uzinduzi huo 
ambapo kiingilo chake ni BURE”
Kampuni ya simu za mkononi ya 
airtel ilianzisha huduma ya UNI255 ili kuendana sambamba na mkakati wao 
wa kusaidia vyuo vikuu nchini kutumia ipasavyo huduma za mtandao ili 
kuboresha sekta ya elimu kwa lengo la kusaidia wateja wake walioko 
vyuoni kufikia malengo yao.

No comments:
Post a Comment