Mwezeshaji
 kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa 
kulia akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
 Bw. Jamhuri David Willium walipomtembelea ofisi kwake wakati wa ziara 
ya Uhamasishaji kwa Vijana kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Vijana leo 
Mkoani Kilimanjaro Wilaya ya Mwanga.
Mkuu
 wa Wilaya ya Mwanga Bw. Shaibu Ndemanga akizungumza na wajumbe kutoka 
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo walipomtembelea ofisini 
kwake kabla ya kwenda kuongea na vijana kutoka Wilaya za Mwanga, Same na
 Moshi vijijini kuwahamasisha na kutoa elimu kuhusu Mfuko wa Maendeleo 
ya Vijana leo Mkoani Kilimanjaro Wilaya ya Mwanga.
Mwezeshaji
 kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa 
akitoa elimu kwa Vijana wa Mwanga, Same, na Moshi Vijijini kuhusu Mfuko 
wa Maendeleo ya Vijana wakati wa uhamasishaji wa Mfuko huo leo Mkoani 
Kilimanjaro Wilaya ya Mwanga.
Baadhi
 ya Vijana kutoka Wilaya za Mwanga, Same na Moshi Vijijini wakifuatilia 
kwa makini elimu iliyokua ikitolewa wakati wa uhamasishaji kuhusu Mfuko 
wa Maendeleo ya Vijana pamoja na mafunzo ya ujuzi na stadi za maisha 
yaliyokua yakitolewa na wahamasishaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, 
Utamaduni na Michezo leo Mkoani Kilimanjaro Wilaya ya Mwanga. 
 
Vijana
 kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Amina Sanga
 akitoa elimu kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa Vijana wa Wilaya 
za Mwanga, Same na Moshi Vijijini leo Mkoani Kilimanjaro.
Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo
………………………………………………………….
Na: Genofeva Matemu – Maelezo
Vijana wametakiwa kujitambua na kuwa na fikra yakinifu na bunifu
 ili kuweza kutatua matatizo yanayowalenga na kuweza kuwa na maamuzi 
katika shughuli wanazozifanya.
Hayo yamesemwa leo na Mwamasishaji kutoka Wizara ya Habari, 
Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Ester Riwa wakati wa semina ya Vijana
 kuhusu uhamasishaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana leo Mkoani 
Kilimanjaro katika wilaya ya Mwanga.
Bibi. Riwa amewashauri vijana kutumia changamoto ya ukosefu wa 
ajira kuwa fursa ya vijana kujishughulisha kwa kujiunga katika vikundi, 
kusajiri vikundi hivyo na kuandika andiko la Mradi litakaowawezesha 
kupata mkopo unaotolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ili waweze 
kuachana na tabia ya kukaa vijiweni na kuweza kuendeleza jamii 
inayowazunguka. 
“Vijana mnapaswa kutimiza wajibu wenu kwa kujishughulisha na 
kuachana na zana potofu yakukaa mitaani mkisubiri kufanyiwa maendeleo na
 serikali ni vyema mkajiunga katika vikundi imara na kufanya kazi kwa 
bidii ili kuweza kujenga taifa letu kwani vijana ni taifa la leo” 
amesema Bibi Riwa.
Akizungumza wakati wa semina hiyo Mkuu wa Kituo cha Vijana 
Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele amewataka vijana kutokuwa na dhana 
potofu ya Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kuwa umewaletea fedha nyingi 
hivyo kuibua miradi mingi isiyokua halisi kwani lengo la mfuko huo ni 
kuwasaidia vijana kuwa na umoja katika kusimamia na kutumia fedha hizo 
kwa makini ili waweze kufikia malengo waliyoyakusudia.
Aidha Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bw. Shaibu Ndemanga ameishukuru 
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuutuma ujumbe uliofika 
Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga kutoa elimu ya uhamasishaji kwa vijana 
kwani vijana wa Mwanga wanahitaji sana elimu hiyo na wao kama viongozi 
wa Wilaya wanajitahidi kuwaelimisha vijana na kuwasaidia pale 
wanapohitaji msaada kutoka kwao.
Akichangia wakati wa semina hiyo Bw. Musa Michumvu kutoka 
Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga amewapongeza wahamasishaji kutoa Wizara 
ya Habari na kuomba elimu hiyo kwa vijana kuendelea kutolewa mara kwa 
mara kwani vijana wanahitaji kuelimishwa ili waweze kuthubutu na 
kujitegemea kwa maendeleo ya jamii na taifa.
No comments:
Post a Comment