TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, January 8, 2015

Shibuda amwagia sifa Waziri Prof. Sospeter Muhongo kuwa mchapakazi na mzalendo

unnamed8V Mbunge wa Maswa Magharibi John Magale Shibuda (kushoto) akitafsiri hotuba ya shukrani iliyotolewa kwa lugha ya kisukuma na mmoja wa wakazi wa kijiji cha Shishiyu mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kabla ya kuzinduliwa rasmi kwa mradi huo.
……………………………………………………………………………………………….
Na Greyson Mwase, Simiyu Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amesema kuwa serikali imetumia shilingi bilioni 25.7 kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji 170 vilivyopo ndani ya mkoa wa Simiyu Alisema hayo alipokuwa akizindua mradi wa umeme vijijini uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili iliyoanza mwaka 2013 inayotarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu. Akifafanua idadi ya vijiji vilivyonufaika na REA Awamu ya Pili Profesa Muhongo alieleza kuwa katika Wilaya ya Bariadi vijiji 45 vilipatiwa umeme, katika Wilaya ya Maswa vijiji 82 vilipatiwa umeme, katika Wilaya ya Busega vijiji 19 vilipatiwa umeme, katika Wilaya ya Itilima vijiji 7 vilipatiwa umeme na katika Wilaya ya Meatu vijiji 17 vilipatiwa umeme. Akizungumzia hali ya usambazaji wa umeme vijijini nchini Profesa Muhongo alisema kuwa vijiji 3734 kati ya vijiji 15,180 ambayo ni asilimia 24.6 vina umeme na kuongeza kuwa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa REA Awamu ya Pili mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu kwa kuongeza vijiji 1500 idadi ya vijiji vyenye umeme itaongezeka na kufikia 5234 ambayo ni sawa na asilimia 34.5. Akizungumzia gharama za uunganishaji wa umeme vijijini Profesa Muhongo alisema kuwa katika REA Awamu ya Kwanza gharama zilishushwa kutoka shilingi 467,000 hadi shilingi 177,000. Alieleza kuwa katika Awamu ya Pili ya REA Serikali ilishusha bei ya uunganishaji wa umeme bila nguzo kutoka shilingi 177,000 hadi shilingi 27,000 ili kuwawezesha wananchi hasa waishio vijijini kuweza kumudu gharama za uunganishaji wa umeme na kuwa na maisha bora. Alisema mara baada ya kukamilika kwa mradi wa umeme vijijini wa REA Awamu ya Pili wananchi ambao wanahitaji umeme nje ya mradi wa REA watalipia shilingi 177,000 tu na iwapo wataona bado wanahitaji umeme chini ya mradi wa REA basi watatakiwa kusubiri awamu nyingine. “ Huduma ya umeme haina itikadi ya kisiasa, kidini ni haki ya kila mwananchi kupata umeme wa uhakika, na sisi kama Serikali tutahakikisha kuwa tunatumia vyanzo vyote vya nishati ili kuwa na umeme wa kutosheleza nchi nzima na kupelekea nchi kuondokana na umasikini.” Alisema Profesa Muhongo. Aliongeza kuwa katika utekelezaji wa mradi wa usambazaji wa umeme vijijini kupitia REA Awamu ya Tatu vijiji vyote nchini vitapatiwa umeme kwa uwiano ulio sawa na kwa awamu tofauti ili kuhakikisha kila wilaya na kijiji kinanufaika na mradi huo. Alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa inatokomeza umasikini kwa watanzania kwa kuwapatia nishati ya umeme kwani ni mhimili mkubwa wa uchumi wa nchi. “Hakuna nchi yeyote duniani iliyoendelea bila kuwa na umeme, tunahitaji umeme kwenye viwanda vyetu, maabara mashuleni, vituo vya afya na katika shughuli nyingine nyingi muhimu za kiuchumi,”alisisitiza Profesa Muhongo Wakati huo huo Mbunge wa Bariadi Magharibi John Magale Shibuda akizungumza kupitia hotuba yake kwenye uzinduzi wa mradi huo alitumia fursa hiyo kumpongeza Waziri wa Nishati na Madini Profesa Muhongo kama kiongozi mchapakazi, mzalendo na mwenye kuitakia mema nchi. Alisema pamoja na Wizara ya Nishati na Madini kukumbana na changamoto mbalimbali lakini Waziri huyo amekuwa imara katika kutekeleza majukumu yake kwa kusimamia vyema sekta ya nishati na madini ambayo ina mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi. “Natumaini ninyi mtakuwa mashahidi wangu, tukiweka tofauti za itikadi za kisiasa, Profesa Muhongo ni mtendaji na ushahidi ni huu usambazaji wa umeme vijijini kwa kasi ya ajabu, kwani kupitia REA Awamu ya Pili vijiji 170 katika mkoa wa Simiyu vimeunganishwa na umeme,’’ alisisitiza Shibuda

No comments:

Post a Comment