.BW. ALFREDY KAPOLE MWENYEKITI WA ALBINO MKOA WA MWANZA AKIZUNGUMZA KATIKA MKOA HUO
WAANDISHI WA HABARI SHEILA SEZI NA GRACE CHILONGOLA WALIPOKUWA WAKIONGEA NA MAMA YAKE NA PENDO
NYUMBANI KWAO NA MTOTO PENDO, 
MWENYEKITI WA ALBINO MKOA WAMWANZA ALFREDY NA MWENYEKITI WA CHAWATA MKOA
 WAKIONGEA NA MAMA PENDO EMMENUEL.
SUNGU SUNGU WAKIMSIKILIZA MKUU WA MKOA
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MWANZA VALENTINO MULOWOLA ALIPOKUWA AKITOA TAARIFA YA UCHUNGUZI HADI SASA
MKUU WA MKOA WA MWANZA MAGESA MULONGO AKIZUNGUMZA NA WANANCHI
…………………………………………………………………………………………
Serikali mkoani Mwanza imesema 
hakuna kulala hadi mtoto Pendo Emmanuel (Albino) apatikane kufatia tukio
 la kutekwa na watu wasio julikana toka tarehe 27.12.2014 katika kijiji 
cha Ndami, Tarafa ya Mwamashimba Wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza na kisha
 kutoweka naye kwenda kusiko julikana hadi sasa.
 MKUU WA MKOA.
 Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo, 
alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji hicho katika mkutano wa 
hadhara uliofanyika kijijini hapo na kuwahusisha wananchi wakijiji hicho
 pamoja na uongozi wa Wilaya na Mkoa huku akitaka kujua hatua 
iliyofikiwa na wana nchi hao katika kuwabaini walifanya unyama huo.
 Mtoto Pendo alitekwa na watu wasiojulikana mnamo usiku wa 
tarehe 27.12.2014 majira ya saa nne usiku akiwa amelala na wazazi wake 
huko Nyumbani kwao na kisha watekaji kutoweka naye na kwenda kusiko 
julikana hadi sasa, huku taarifa za Polisi zikionesha jumla ya watu kumi
 na watano (15), wakiendelea kushikiliwa na jeshi la Polisi kwa ajili ya
 mahojiano zaidi.
 Akihutubia wananchi wa kijiji hicho Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, 
alisema ni tukio la kusikitisha kwani toka mwaka 2007 hakuna tukio la 
namna hiyo lililo wahi kutokea katika Wilaya hiyo na tukio la mwisho 
lililotokea lilimkumba mwananchi wa Wilaya hiyo aliyekuwa amesafiri 
kwenda Mkoani Shinyanga kwa shughuli zake.
 Amesema kiburi walicho nacho watekaji hakiwezi kuwa nje ya 
mipaka ya kijiji hicho cha Ndami bali mpango mzima unajulikana kwa 
wenyeji na ndio maana ilikuwa rahisi kufanya unyama huo “Kiburi cha 
watekaji kimo humu humu haiwezekani mtu kutoka mbali aje atekeleze tukio
 hapa kijijini bila yakuwa na wenyeji lazima kuna mtu au watu 
walioshirikiana na wahalifu hao”, alisema Mulongo na kuongeza “ kwa 
mazingira ya Nyumba ya kina Pendo ilipo kule hakuna sehemu yakutokea na 
kama mliona pikipiki inaranda randa mchana,.. iweje mshindwe kuitilia 
shaka? Hapana,  hii haikubaliki! mimi nimekuja kuwaambia nataka Pendo 
apatikane na sio vinginevyo, nawapa siku tano ijumaa nitarudi hapa 
mniambie Pendo yuko wapi! Alisema mkuu huyo wa Mkoa akionesha 
kusononeshwa na tukio hilo.
 “Mbona mifugo inapo ibwa inapatikana”? Aliwahoji viongozi wa 
sungu sungu na kusema haiingii akilini kusema wakati wa tukio la utekaji
 sungu sungu wote walikuwa wamekwenda kula chakula na ndipo kadhia hiyo 
ilipotokea, mkuu wa mkoa, alihoji kufatia kauli iliyotolewa na kiongozi 
wa sungu sungu kuwa wakati wa tukio askari wote wa sungu sungu walikuwa 
wamekwenda kula majira ya saa tatu na tukio kutokea saa nne.
 MWENYEKITI WA ALBINO MWANZA.
 Awali akielezea kusikitishwa kwake na tukio hilo, Mwenyekiti wa
 chama cha watu wenye ulemavu wa Ngozi mkoani hapa Alfred Kapole, 
alisema inasikitisha kuona wanadamu wakiwauwa binadamu wenzao kama vile 
wanyama bila hata woga na vyombo vya maamuzi vikishindwa kutoa hukumu 
kwa wakati huku akielekeza lawama zake kwa mahakama na Mkemia Mkuu. “Mh.
 Mkuu wa mkoa inasikitisha kuona miongoni mwa kesi 72 zilizokuwa 
mahakamani, ni kesi 3 tu ndizo zilizokwisha kutolewa hukumu” alisema 
Kapole, na kuongeza ingekuwa ni kesi ya Wabunge wameshindana kwenye 
masuala ya uchaguzi ingekuwa imekwisha hukumiwa lakini kwakuwa ni 
mlemavu wa ngozi,   basi kupuuzia kumekuwa kwingi mno. Alisema kapole.






No comments:
Post a Comment