Mbunge wa Jimbo la Chalinze, 
Ridhiwani Kikwete (katikati) akikabidhi gari jipya la kubebea wagonjwa 
(Ambulance), kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo,Dk. Mastidia Rutaihwa
 kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Chalinze, katika mkutano wa hadhara 
uliofanyika mjini Chalinze jioni hii. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni 
Mganga Mkuu wa kituo hicho, Dk. Bamba Victor na Diwani wa Kata ya 
Bwilingu, Nasa Karama. 
 Muumini wa Dini ya Kikiristo, 
Heema Said akitoa neno la shukrani kwa Mbunge wa Jimbo la 
Chalinze,Ridhiwani Kikwete 9aliyevaa koti kushoto) alipokabidhi 
ambulance hiyo. Ridhiwani alisema kuwa yeye hivi sasa ni mbunge wa vyama
 vyote jimbo humo hivyo ambulance aliyoitoa itoe huduma kwa wakazi wote 
wa jimbo hilo bila kubagua watu kutokana na itikadi zao. Pia aliuasa 
uongozi wa kituo hicho cha afya na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya 
Bagamoyo kuhakikisha wanatunza vizuri gari hilo.
 Dok Rtaihwa akimkabidhi ufunguo 
wa gari hilo Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Chalinze, Dk.Victor baada
 ambulance hiyo kukabidhiwa na Mbunge Ridhiwani.
 Dk. Victor akitoa shukurani kwa Mbunge Ridhiwani kwa msaada huo wa ambulance
 Wakifurahia kwa pamoja kupata usafiri huo muhimu kwa wagonjwa
 Mbunge Ridhiwani Kikwete na Dk. Rutaihwa wakiangalia ndani ya ambulance hiyo
 Wakiwa na furaha baada ya kuangalia samani zilizomo ndani ya ambulance hiyo
 Ridhiwani  pamoja na viongozi wa 
dini ya kiislamu wakiliombea dua gari hilo. Kutoka kulia ni Alhaji  
Sheikh Hussein Fuko na Alhajj Khamis Magula
 Ridhiwani 9katikati) na Mbuunge 
wa Jimbo la Mtera, Lusinde wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya 
watumishi wa Kituo cha Afya cha Chalinze akiwemo Mganga Mkuu wa Wilaya 
ya Bagamoyo, Dk. Rutaihwa.
 Mganga Mkuu wa Wilaya ya 
Bagamoyo, Dk.Mastidia Rutaihwa akitoa shukurani kwa Ridhiwani kwa msaada
 wa Ambulance na kuahidi kuitunza
 Ridhiwani akipongezwa na wananchi kwa kuwapatia ambulance
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya Hafsa Kazinja akicheza muziki na mmoja wa wazee wa Chalinze alipotumbuiza katika mkutano huo
 Ridhiwani akihutubia katika mkutano huo
 Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria makabidhiano ya ambulance katika viwanja vya miembe saba mjini Chalinze 
 Mbunge wa Jimbo la Mtera, Dodoma,
 Lusinde ambaye alikuwa safarini akitokea Dodoma kwenda Dar kwenye vikao
 vya Kamati za Bunge, aliamua kushiriki kwenye mkutano huo ambapo 
alimsifia Mbunge Ridhiwani kwa kipindi kifupi alichoaguliwa kuwa mbunge 
miezi sita iliyopita kutekeleza kwa kiasi kikubwa ahadi alizozitoa 
wakati wa kampeni ikiwemo ambulance hiyo, ujenzi wa visima katika vijiji
 mbalimbali na ujenzi wa barabara pamoja na zahanati
Lusinde akikumbatiana kwa furaha na Ridhiwani baada ya mkutano huo kumalizika
No comments:
Post a Comment