Mbunge wa Jimbo la Chalinze, 
Ridhiwani Kikwete,akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha
 Fukayosi, Kata ya Fukayosi, wakati wa ziara ya kikazi pamoja na 
kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge miezi  sita 
iliyopita.Ridhiwani kutoruhusu hata kipande cha heka moja kuporwa na 
matapeli katika jimbo lake la Chalinze.
 Kijana Salumu Khamis akiuliza swali mbele ya Mbunge Ridhiwani Kikwete kuhusu tatizo la maji katika Kijiji cha Fukayosi
 Mkuu wa Miradi wa Mkoa wa Pwani 
wa Tanesco, Leo Mwakatobe, akielezea jinsi umeme utakavyosambazwa katika
 Kijiji cha Fukayosi na vijiji vingine Jimbo la Chalinze.
 Mwenyekiti mpya wa Serikali ya 
Kijiji cha Fukayosi, Salum Mkwecha akimshukuru mbunge kwa ahadi 
mbalimbali alizozitoa katika miradi mbalimbali katika kijiji hicho.
 Ridhiwani akibadilishana mawazo 
na mmoja wa watawa baada ya kumalizika kwa mkutano katika Kijiji cha 
Fukayosi Jimbo la Chalinze.
 Mwenyekiti mstaafu wa Kata ya 
Fukayosi,Adam Masoud  akimuomba Mbunge Ridhiwani kuhikisha anaweka 
miundombinu ya barabara na maji na masuala ya afya katika Kijiji cha 
Mkenge,wakati wa ziara yake katika Kata ya Fukayosi ya kuwashukuru kwa 
kumchagua pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuangalia jinsi ya 
kuzitafutia ufumbuzi.
 Mkazi wa Kijiji cha Mkenge, 
Khamis Mwanga akielezea kero ya barabara ya Mwavi hadi Mkenge ambayo 
alidai inarudisha nyuma maendeleo ya kijiji hicho hivyo kumtaka 
Ridhiwani awasaidia kuijenge barabara hiyo ili iweze kupitika bila 
matatizo katika vipindi vyote. Ridhiwani aliwajibu kuwa tayari barabara 
hiyo imepata mkandarasi anayetarajia kuanza kazi katika siku chache 
zijazo.
 Katibu wa CCM Tawi la Mkenge, 
Omar Seleman akimuomba Mbge Ridhiwani asaidie kumalizia ujenzi wa 
msikiti wa Mkenge, Ombi ambalo alilikubali na kuahidi kupaua kwa gharama
 zake.
 Ridhiwani akijibu maswali mbalimbali ya wananchi wakati wa mkutano katika Kijiji cha Mkenge
 Ridhiwani akikagua maendeleo ya 
ujenzi wa msikiti wa Mkenge ambao ameahidi kuchangia mabati na mbao za 
kupaua jengo hilo la ibada.
 Mwenyekiti wa CCM Kata ya 
Fukayosi, Olnjurie Marigwa akihtubia katika mkutano uliofanyika katika 
kijiji cha Mwavi, Kata ya Fukayosi
 Masoud Fundikira akimuomba Mbunge
 wao Ridhiwan, anzishe mashindano ya mpira wa miguu kuwania kikombe cha 
Ridhiwani Cup ili kuendeleza michezo katika jimbo hilo. Ridhiwani 
alilikubali ombi hilo kwa kuanzia kutoa misaada ya mipira na jezi katika
 kila timu ya kata za jimbo hilo.
 Ridhiwani akihutubia katika 
Kijiji cha Mwavi ambapo aliahidi kufuatilia kwa karibu kuhusu suala la 
alilogawiwa Mkorea ili kijiji cha mwwavi kipate haki.
 Katibu wa CCM Wilaya ya Bagamoyo 
Kombo Kamote, akiwafunda viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Mwavi 
waliochaguliwa hivi karibuni ili wawatendee haki wananchi.
 Ridhiwani akihutubia katika 
mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Kidomole, ambapo aliwajia juu 
anaowaita matapeli wanaouza ardhi katika Jimbo la Chalinze bila kufuata 
sheria na utaratibu. Alisema kuwa hayuko tayari kuona hata heka moja ya 
jimbo hilo ikikuzwa bila utaratibu.
Ridhiwani akiagana na Meya wa  Morogoro, Amir Nondo ambaye ni mzaliwa wa Kata ya Kiwangwa katika jimbo hilo la Chalinze.
No comments:
Post a Comment