Makamu
 wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akifungua pazia 
kuashiria ufunguzi wa wodi mpya ya wagonjwa mahututi (ICU) katika 
Hospitali Kuu ya Mnazimmoja ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya miaka 
51 ya Mapinduzi ya Zanzibar. (Picha zote na Makame Mshenga-Maelezo 
Zanzibar). 
Sehemu
 ya vitanda vya wodi mpya ya wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali 
Kuu ya Mnazimmoja. (Picha zote na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
Sehemu
 ya vitanda vya wodi mpya ya wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali 
Kuu ya Mnazimmoja. (Picha zote na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
Makamu
 wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad wa tatu kutoka 
(kushoto) akionyeshwa kifaa maalum cha kusaidia wagonjwa  mahututi 
wanapolazwa katika wodi hiyo. (Picha zote na Makame Mshenga-Maelezo 
Zanzibar). 
Waziri
 wa Afya Rashid Seif akitoa taarifa juu ya wodi mpya ya wagonjwa 
mahututi kabla ya kumkaribisha Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar 
kuzungumza na walikwa katika hafla hiyo. 
Makamu
 wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na 
wafanyakazi na wageni waalikwa katika ufunguzi wa wodi mpya ya ICU 
katika Hospitali  Kuu ya Mnazimmoja Mjini Zanzibar. 
 Baadhi ya Wafanyakazi wa sekta ya Afya wakimsikiliza Makamu wa Kwanza 
wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad wakati wa ufunguzi wa wodi 
ya wagonjwa mahututi (ICU). Hafla hiyo imefanya Hopitali Kuu ya 
Mnazimmoja Mjini  Zanzibar.  
Maalim
 Seif Sharif Hamad akiagana na Mkurugenzi wa Hospitali Kuu ya Mnazimmoja
 Dkt. Jamala baada ya ufunguzi wa wodi ya wagonjwa mahututi (ICU).(Picha
 zote na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
………………………………………………………………………….
Na Miza Kona na Abdulla Ali –Maelezo Zanzibar   
arif Hamad amewataka wauguzi 
kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wabadilike kifikra na 
mawazo katika kutekeleza majukumu yao.
Hayo ameyaeleza katika Hospitali 
kuu ya Mnazi Mmoja Wilaya ya Mjini Unguja wakati wa Ufunguzi wa Wodi 
mpya ya Wagonjwa Mahututi (ICU) ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha 
miaka 51 ya sherehe ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Amesema wauguzi wana dhamana kubwa
 ya kuokoa maisha ya watu hivyo wanajukumu la kuhakikisha wanatoa huduma
 iliyo bora na ya uhakika.
Maalim  Seif amesema wauguzi wa 
wagonjwa mahututi (ICU) wana haki ya kupata mafunzo ili waweze kutoa 
huduma hiyo kwa ufanisi wa hali ya juu ili kufikia lengo lililokusudiwa.
“Wafanyakazi kuwa wapole, wenye 
kutumia lugha nzuri kwa wagonjwa, kuwa wastahamilivu na waliotayari 
katika kutoa huduma zao”, amesema Maalim Seif.   
Amewataka wafanyakazi wa ICU kuwa 
wawazi katika kutoa taarifa zinazohusu maendeleo ya wagonjwa pale 
inapohitajika ili kuondosha usumbufu kwa ndugu na jamaa wanapotaka 
kupata taarifa hizo.
Aidha amewataka wananchi kufuata taratibu zilizowekwa ili kuepusha usumbufu na matatizo zaidi kwa wagonjwa wa sehemu hiyo.
Maalim Seif amewataka wananchi 
kutumia vyema huduma hiyo muhimu ili iweze kudumu na kupunguza gharama 
za usafirishaji wa wagonjwa hao kufuata huduma nje ya nchi.
Mapema Waziri wa Afya Seif Rashid 
Suleiman amesema huduma ya ICU ni muhimu kwa ajili ya kuokoa maisha ya 
watu na ni lazima ipate zana za uchunguzi za uhakika ili kuweza kufanya 
matibabu ya uhakika na usahihi.
Amefahamisha kuwa Wizara imeandaa 
mpango maalum wa kuratibu dawa zinazotumika nchini kupitia Bohari Kuu ya
 dawa na Mfamasia mkuu wa serikali kuwacha kuagiza dawa zisizotumika ili
 kupunguza gharama na hasara.
Nae Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dr.
 Mohamed Saleh Jidawi amesema Wodi ya ICU ina vifaa vya kutosha na 
huduma zote zinapatikana bila ya usumbufu katika wodi hiyo.
Wodi hiyo imegharimu zaidi ya Dola
 millioni moja hadi kukamilika kwake ambayo ina vitanda nane na 
inajitosheleza kwa huduma zote zinazohitajika kwa wagonjwa.

No comments:
Post a Comment