TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, January 10, 2015

MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA ZANZIBAR MAALIM SEIF SHARIF HAMAD AFUNGUA CHUMBA CHA WAGONJWA MAHTUTI (ICU) SPITALI KUU MNAZI MMOJA.

unnamed1c
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akifungua pazia kuashiria ufunguzi wa wodi mpya ya wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar. (Picha zote na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar). unnamed2cSehemu ya vitanda vya wodi mpya ya wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja. (Picha zote na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
unnamed3cMakamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad wa tatu kutoka (kushoto) akionyeshwa kifaa maalum cha kusaidia wagonjwa  mahututi wanapolazwa katika wodi hiyo. (Picha zote na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar). unnamed4cWaziri wa Afya Rashid Seif akitoa taarifa juu ya wodi mpya ya wagonjwa mahututi kabla ya kumkaribisha Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kuzungumza na walikwa katika hafla hiyo. unnamed5cMakamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na wafanyakazi na wageni waalikwa katika ufunguzi wa wodi mpya ya ICU katika Hospitali  Kuu ya Mnazimmoja Mjini Zanzibar. unnamed6c Baadhi ya Wafanyakazi wa sekta ya Afya wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad wakati wa ufunguzi wa wodi ya wagonjwa mahututi (ICU). Hafla hiyo imefanya Hopitali Kuu ya Mnazimmoja Mjini  Zanzibar.  unnamed7cMaalim Seif Sharif Hamad akiagana na Mkurugenzi wa Hospitali Kuu ya Mnazimmoja Dkt. Jamala baada ya ufunguzi wa wodi ya wagonjwa mahututi (ICU).(Picha zote na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
………………………………………………………………………….
Na Miza Kona na Abdulla Ali –Maelezo Zanzibar  
arif Hamad amewataka wauguzi kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wabadilike kifikra na mawazo katika kutekeleza majukumu yao.
Hayo ameyaeleza katika Hospitali kuu ya Mnazi Mmoja Wilaya ya Mjini Unguja wakati wa Ufunguzi wa Wodi mpya ya Wagonjwa Mahututi (ICU) ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha miaka 51 ya sherehe ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Amesema wauguzi wana dhamana kubwa ya kuokoa maisha ya watu hivyo wanajukumu la kuhakikisha wanatoa huduma iliyo bora na ya uhakika.
Maalim  Seif amesema wauguzi wa wagonjwa mahututi (ICU) wana haki ya kupata mafunzo ili waweze kutoa huduma hiyo kwa ufanisi wa hali ya juu ili kufikia lengo lililokusudiwa.
“Wafanyakazi kuwa wapole, wenye kutumia lugha nzuri kwa wagonjwa, kuwa wastahamilivu na waliotayari katika kutoa huduma zao”, amesema Maalim Seif.   
Amewataka wafanyakazi wa ICU kuwa wawazi katika kutoa taarifa zinazohusu maendeleo ya wagonjwa pale inapohitajika ili kuondosha usumbufu kwa ndugu na jamaa wanapotaka kupata taarifa hizo.
Aidha amewataka wananchi kufuata taratibu zilizowekwa ili kuepusha usumbufu na matatizo zaidi kwa wagonjwa wa sehemu hiyo.
Maalim Seif amewataka wananchi kutumia vyema huduma hiyo muhimu ili iweze kudumu na kupunguza gharama za usafirishaji wa wagonjwa hao kufuata huduma nje ya nchi.
Mapema Waziri wa Afya Seif Rashid Suleiman amesema huduma ya ICU ni muhimu kwa ajili ya kuokoa maisha ya watu na ni lazima ipate zana za uchunguzi za uhakika ili kuweza kufanya matibabu ya uhakika na usahihi.
Amefahamisha kuwa Wizara imeandaa mpango maalum wa kuratibu dawa zinazotumika nchini kupitia Bohari Kuu ya dawa na Mfamasia mkuu wa serikali kuwacha kuagiza dawa zisizotumika ili kupunguza gharama na hasara.
Nae Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dr. Mohamed Saleh Jidawi amesema Wodi ya ICU ina vifaa vya kutosha na huduma zote zinapatikana bila ya usumbufu katika wodi hiyo.
Wodi hiyo imegharimu zaidi ya Dola millioni moja hadi kukamilika kwake ambayo ina vitanda nane na inajitosheleza kwa huduma zote zinazohitajika kwa wagonjwa.

No comments:

Post a Comment