Mkurugenzi
 Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati, Maji na Mafuta (Ewura), Felix 
Ngamlagosi (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari 
ofisini kwake Dar es Salaam leo, kuhusu mwenendo wa bei za mafuta nchini
 na katika soko la Dunia. Kulia ni Mkurugenzi wa Petroli, Godwin Samwel.
Mkurugenzi wa Petroli, Godwin Samwel (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
 Ofisa Mawasiliano wa Ewura, Titus Kaguo (kushoto), akizungumza katika mkutano huo.
 Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
 ………………………………………………………………………………………….
Dotto Mwaibale
MAMLAKA
 ya Udhibiti wa Nishati, Maji na Mafuta (Ewura), imepunguza bei za 
mafuta kote nchini kuanzia leo kutokana na kudorora kwa uchumi wa bara 
la ulaya.
Hayo
 yalibainishwa  na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati, 
Maji na Mafuta (Ewura), Felix Ngamlagosi wakati akizungumza na waandishi
 wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo mchana, kuhusu mwenendo wa 
bei za mafuta nchini na katika soko la Dunia.
Alisema
 kuanzia leo bei ya mafuta ya petroli kwa lita moja itauzwa sh.1955 na 
hiyo inatokana na kushuka kwa jumla ya asilimia 16 sawa na pungufu kwa 
jumla ya sh.311 kwa lita.
 Alisema
 bei ya petroli katika soko la dunia imeshuka kwa jumla ya aasilimia 25 
kuanzia Julai hadi Novemba 2014, sawa na pungufu kwa jumla ya dila 249 
kwa tani.
Ngamlagosi
 alisema mafuta ya dizeli kwa lita moja yatauzwa sh.1846 na kuwa bei 
hiyo imeshuka kwa asilimia 13 sawa na pungufu kwa jumla ya sh.244 kwa 
lita na kuwa dizeli kwa soko la dunia imeshuka kwa jumla ya asilimia 28 
kuanzia Julai hadi Novemba 2014 sawa na pungufu kwa jumla ya dola 189 
kwa tani na kuwa mafuta ya taa yatauzwa sh. sh.1833 kwa lita.
Alisema
 katika kipindi cha robo ya mwisho wa mwaka kuanzia mwezi Septemba hadi 
Desemba 2014, bei za mafuta ghafi zimekuwa zikishuka kwa kasi 
ikilinganishwa na kipindi cha hapo nyuma ambapo zimeshuka toka dola 100 
kwa pipa hadi kufikia wastani wa dola 60 kwa pipa moja ambayo ni sawa na
  karibu asilimia 40.
Alisema
 viwango hivyo vya bei iliyopungua ni katika soko la Dar es Salaam na 
mikoa mingine bei zao zimepangwa kutokana na kuwepo kwa gharama za 
usafirishaji.
Ngamlagosi
 alitoa mwito kwa wanunuaji wa mafuta hayo kuhakikisha wanapatiwa lisiti
 baada ya kununua kwani itasaidia kuwabaini wafanyabiashara wasio 
waaminifu ambao wataendelea kuuza kwa bei ya zamani.
“Natioa
 mwito wa kuwaomba wanunuaji wa mafuta kuhakikisha wanapewa lisiti kwani
 itatusaidia kuwabaini wale wanauza kwa bei ya juu, na pia itamsaidia 
mnunuzi iwapo atauziwa mafuta yaliyochini ya kiwango na ukusanyaji wa 
kodi ya serikali” alisema Ngamlagosi.
Naye
 Mkurugenzi wa Petroli, Edwin Samwel alisema Ewura imejipanga vizuri 
kuhakikishha hakuna ujanja ujanja utakaojitokeza wa kudai mafuta 
yamekwisha au yaliyopo yatauzwa kwa bei yaliyonunuliwa.
Alisema
 mfanyabiashara yeyote atakayekiuka utaratibu huo atachukuliwa sheria 
pamoja na kufungiwa biashara yake ingawa alisema hali hiyo 
haitajitokeza. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)
No comments:
Post a Comment