Yote Uliyowahi Kutaka Kujua Kuhusu Mkito.com:
Mahojiano Na Mwanzilishi Mwenza,Sune Mushendwa
Kwa miaka nenda rudi, wasanii wa 
kitanzania walikuwa na kilio kinachofanana. Ungekaa pembeni bila 
kuwaona, ungedhani kutokana na mwangwi wa kilio chao, anayelia ni mmoja.
 Hapana. Wote walikuwa [na pengine bado wanaendelea kulia] kutokana na 
kunyonywa “jasho lao”.
Kimsingi “jasho” wanalolilia 
limekuwa ni soko na usambazaji. Kipaji unacho na watu wanakubali kazi 
zako. Tatizo utaifikishaje kazi yako kwa mashabiki zako? Ni wazi kwamba 
unahitaji msaada wa kimasoko na usambazaji. Kusema utaweza kufanya kila 
kitu peke yako ni kujidanganya.Nani? Yupo wapi na utampa kazi zako kwa 
thamani gani? Kilio chao kilianzia hapo. Wengine wakaamua kuachana na 
muziki [wengine muziki umewaacha wao] kutokana na ukosefu wa soko la 
uhakika na kuona kadhaa ya kupanga foleni ukisubiri “hela yako”.
Mabadiliko ya masoko ya kazi za 
wasanii duniani kutoka kwenye mifumo ya ki-analojia kwenda kwenye 
dijitali na pia kutoka katika mifumo ya vitu kama CD mpaka kwenda kwenye
 matumizi ya simu na vikabrasha vingine vya mikononi, kulimaanisha 
kwamba soko la wasanii wa kitanzania [na Afrika kwa upana wake] lilikuwa
 linazidi kufifia. Hakuna tena shabiki anayetaka kubeba furushi la CD. 
Inakuwaje?
Hapo ndipo baadhi ya vijana 
wakaona fursa kuthibitisha kwamba penye tatizo ndipo pa kukimbilia.Fursa
 ni kama dhahabu au almasi.Huwezi kuiokota kando ya bahari ikiwa 
imetupwa ufukweni na mawimbi ya bahari. Wazo la fursa likazaa Mkito.Com 
mahali ambapo wasanii sasa wanapumua na huku changamoto pekee ni 
kuwashawishi mashabiki kupakua kazi zao kutoka Mkito.Com. Kila mara 
shabiki anapofanya hivyo, msanii ananufaika na kupata nguvu zaidi ya 
kuingia tena studio kunogesha mambo. It’s a win win situation.
Sune Mushendwa [pichani juu] ni 
mwanzilishi-mwenza wa Mkito.Com. Kujua mengi zaidi nilimtafuta na kupiga
 naye story kidogo. Ameelezea mengi. Nakukaribisha usome mahojiano yangu
 naye ili ujue yote ambayo umekuwa ukitaka kuyajua kuhusu Mkito.Com 
.Twende pamoja;
BC: Sune karibu sana ndani ya 
BongoCelebrity. Hii ni mara yako ya kwanza hapa na bila shaka wasomaji 
wangependa kupata japo kwa kifupi tu historia yako. Ulizaliwa 
wapi,ukakulia wapi na kusomea wapi na mambo kama hayo
SM: Asante sana kwa 
kunikaribisha. Mimi nimekulia Arusha na ndipo niliposoma pia. Baada ya 
sekondari nilienda kusoma chuo kikuu nchini Finland ambako mama yangu 
ndipo anapotokea.
BC: Wajasiriamali wengi ambao 
nimewahi kufanya nao mahojiano huniambia kwamba waliamua kufanya 
wanachokifanya baada ya kukosa au kubughudhiwa na kitu fulani.Huwa kuna 
kisa au mkasa nyuma ya pazia. Kwa upande wa Mkito kuna kisa au mkasa 
wowote? Ilikuwaje mpaka ukasema Aha…Mkito ikaanza? Na hili jina lilikuja
 namna gani?
SM: Baada ya 
kutoka masomoni nilianzisha studio ya muziki Arusha.Lakini tatizo kubwa 
lililoonekana moja kwa moja ni kwamba wasanii pamoja na studio zinapata 
tabu sana katika kusambaza na kuuza kazi zao. Niliona tunahitajika njia 
ya kuweza kusambaza muziki kirahisi na pia kuingiza kipato kwa msanii. 
Baada ya research na maandalizi ya zaidi ya miaka 4 ndipo Mkito.com 
ilipozaliwa tarehe 30 April 2014.
BC: Mpaka sasa Mkito imefanikiwa kuwa na wasanii wangapi? Nini masharti ya msanii kujiunga au kuweka kazi zake katika Mkito?
SM: Kuna wasanii 
takriban 600 waliojiunga mpaka sasa na wanaongezeka kila siku. Masharti 
ya kujiunga ni marahisi, uwe umerekodi wimbo anghalau mmoja wenye ubora.
 Baada ya hapo msanii anaweza kujitengenezea akaunti yake kupitia tovuti
 www.mkito.com na 
kupakia[upload] nyimbo zake mwenyewe. Msanii baada ya hapo anaweza 
kufuatilia mauzo yake mwenyewe kupitia akaunti yake aliyoitengeneza.
BC: Bado nikiwa katika swali au 
maswali ya wasanii. Msanii akishaingia katika mkataba au makubaliano na 
ninyi, bado anakuwa na haki na uhuru wa kuendelea kusambaza kazi zake 
katika platforms zingine kama vile iTunes,Spotify,Google Play nk?

No comments:
Post a Comment