TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, January 9, 2015

Rais Jakaya Kikwete kuzindua nyumba mpya za makazi ya Wanajeshi Gongolamboto

index
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linatoa taarifa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete atazindua nyumba mpya za makazi ya Wanajeshi eneo la Gongolamboto mnamo tarehe 10 Januari, 2015,    Saa 3:00 Asubuhi.
 
Aidha, uzinduzi wa nyumba hizo ni sehemu ya nyumba elfu kumi za  mwanzo za makazi ya Maafisa na Askari wa JWTZ zilizojengwa katika mikoa mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kuondoa tatizo la nyumba za makazi kwa Wanajeshi.
 
Ujenzi wa nyumba hizo za kisasa umefanywa na Kampuni iitwayo ‘Shanghai Construction Group’ ya Jamhuri ya watu wa China.
 
Waandishi wa Habari wanaombwa kuhudhuria na kufanya ‘Coverage’ katika tukio hili muhimu.
   
  Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga

No comments:

Post a Comment