Mbunge wa Jimbo la Chalinze, 
Ridhiwani Kikwete akihutubia wananchi mjini Chalinze, Wilaya ya 
Bagamoyo, Pwani jana, ambapo pamoja na kuwashuru kwa kumchagua, pia 
alisema atatumia uanasheria wake kuwasaidia baadhi ya wakazi wa jimbo 
hilo wanaonyimwa haki zao za msingi ikiwemo kuporwa ardhi.
 Ridhiwani akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo uliofanyika katika Uwanja wa Masoko mjini Chalinze
 Mkazi wa Chalinze, Bibi akitoa 
malalamiko yake mbele ya Mbunge Ridhiwani Kikwete ya kudhulumiwa shamba 
lake na watu wasiojulikana.
 Mkazi wa Chalinze Methodius 
Kaijage, akiuliza swali kuhusu alama za x zilizowekwa kwenye nyumba zao 
kwa ajili ya upanuzi wa barabara ambazo alidai ni takribani miaka kumi 
imepita bila kupewa fidia hivyo kusababisha kukosa maendeleo.
 Sehemu ya wakazi wa Kata ya Bwilingu, wakiwa katika mkutano na mbunge wao mjini Chalinze.
 Ridhiwani akihutubia wananchi katika Kitongoji cha Chalinze Mzee wakati wa ziara ya kuwashukuru wananchi na kusikiliza kero zao
 Ridhiwani akimsalimia mmoja wa wazee wa Kitongozi cha Chalinze Mzee
 Mmoja wa vijana wa Chalinze Mzee akiuliza swali
 Mzee Ibrahim Koga akielezea mbele ya Mbunge asivyotendewa haki na Baraza la Kata ya Bwilingu la kuporwa ardhi yake
Mama mwenye Jamii ya Kimasai 
Rehema Lazaro akilalamika mbele ya mbunge kitendo cha baadhi ya wananchi
 kutoa lawama kwa wafugaji wote badala ya wafugaji wanaofanya vurugu kwa
 kupeleka mifugo kwenye mashamba ya wakulima na kuchafua visima vya 
maji.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
No comments:
Post a Comment