TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, January 4, 2015

Chamijata yapata msaada wa mabao kutoka kwa Diwani

indexMwandishi Maalum
DIWANI wa Kata ya Msongola Angelina Malembeka ametoa msaada wa mabao matatu kwa Chama cha Michezo ya Jadi Tanzania (Chamijata) ikiwa ni jitihada zake za kuendeleza mchezo huo.
Malembeka ambaye pia ni Katibu wa Madiwani wa Manispaa ya Ilala alikabidhi mabao hayo jana katika ofisi za Chamijata zilizipo Temeke jijini Dar es Salaam.
Alisema ameamua kutoa msaada huo kwa Chamijata kutokana na kuona kwa muda mrefu mchezo huo umeshindwa kuvuma hivyo kwa kuanzia mabao hayo yatawasaidia.
Diwani huyo alisema pia katika kuendeleza mchezo huo amegawa mabao katika mitaa tisa ya Kata yake lengo likiwa ni kuendeleza mchezo huo kuanzia Mitaa hadi ngazi ya Taifa.
“Jamani naomba mpokee mabao haya ila naahidi kuendelea kuwasaidia pale msaada utakapo hitajika kwani mimi ni mdau  wa michezo hasa michezo ya jadi,” alisema Malembeka.
Malembeka alisema iwapo michezo ya jadi itapewa kipaumbele ni dhahiri kuwa jamii itadumisha tamaduni zake kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Chamijata Gamaliel Mhanga alimshukuru Diwani huyo kwa msaada wa mabao hayo ambapo aliwaomba wadau wengine kujitokeza kusaidia chama hicho.
Mhanga alisema Chamijata imejipanga kutekeleza mipango yake mbalimbali ya kuboresha na kuendeleza michezo ya jadi kwa kushirikiana na wadau kama Diwani Malembeka.

No comments:

Post a Comment