TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, January 10, 2015

MAONYESHO YA BIASHARA YAFUNGULIWA ZANZIBAR

indexMakamu wa Pili wa  Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema lengo  la kuandaa  Tamasha la Biashara Zanzibar ni kushajihisha ukuwaji wa Uchumi  na kuirejeshea Zanzibar hadhi yake ya zamani  ya kuwa kituo kikuu cha Biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Amefahamisha kuwa Tamasha hilo ambalo litawakutanisha Wafanya Biashara wakubwa kutoka Zanzibar na sehemu nyengine  litatoa fursa  kwa wafanya biashara wadogo  na wanunuzi wengine wa kawaida kupata bidhaa muhimu kwa bei ya kawaida.
Hayo aliyasema wakati wa ufunguzi wa Tamasha la Pili la  Biashara la mwaka 2015 huko katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za kutimiza  miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
“Wafanya Biashara na Wajasiria Mali waitumie fursa hii adhimu ipasavyo kwa lengo la kuendeleza Biashara hapa Zanzibar na kupata huduma muhimu”Alisema Balozi Seif.
Balozi Seif alifahamisha kuwa Matamasha ya Biashara  hutoa   fursa ya kukuza Sekta ya Utalii  kwa   kuhudhuriwa na wageni mbali mbali kutoka nje.
Alisema  nchi nyingi Duniani zinafaidika na Matamasha makubwa ya kibiashara kama vile Tamasha la Dubai Shoping  Festival linalokusanya zaidi ya Wageni Milioni 4.4 na kuchangia pato la Taifa zaidi ya Bilioni 15.
Alieleza kuwa Serikali  itaendelea kushirikiana na Wafanya Biashara wa Zanziba,r Tanzania na Afrika  Mashariki katika kuhakikisha sekta ya Biashara inazidi kukua na kuimarika  ili kuongeza pato la Taifa .
Sambamba na hayo alisema Serikli itaendelea kushughulikia  changamoto zinazoikabili Sekta ya Biashara kama vile upatikanaji wa vifungashio, kuanzisha mfumo  wa nambari za utambulisho wa bidhaa (barcodes) na  kufikia Viwango vya Biashara Kimataifa.
“Ni vyema Matamasha ya  aina hii yakajumuisha maonyesho ya Utamaduni wa Mzanzibari zikiwemo kazi za Sanaa, Vyakula vya asili na Muziki wa mwambao ambao unaendelea  kutoweka” Alisema Makamu wa Pili.
Ameitaka Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko kulitangaza zaidi Tamasha la Biashara na kuanzisha eneo maalum la maonyesho ya Biashara  hapa Zanzibar.
Balozi Seif alitoa shukurani zake kwa Taasisi za Serikali na  watu binafsi, Makampuni, Wafanya Biashara  wa ndani na nje ya nchi kwa  kushiriki  Tamasha hilo.
Nae Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko  Nassor Ahmed Mazurui  alisema  zaidi ya Wafanya Biashara  160 watashiriki Tamasha la mwaka huu.
Alisema Tamasha hilo linalengo la kuitangaza Zanzibar Kiutalii na Kibiashara kwa kuandaa  mazingira mazuri  ili kuleta kivutio kikubwa kwa  washiriki na wanunuzi. 

No comments:

Post a Comment