TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 6, 2015

UADILIFU NDIYO KIGEZO MUHIMU CHA UONGOZI UCHAGUZI UJAO

 
1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi mbalimbali waliohudhuria kwenye mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Tangamano mjini Tanga, katika mkutano huo Kinana ametumia muda mwingi kuwashukuru wananchi wa mkoa wa Tanga na watanzania kwa ujumla kwa kukiamini chama cha Mapinduzi na kukipa ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Disemba 14 mwaka jana ambapo Chama cha Mapinduzi mkoa wa Tanga kimeshinda kwa asilimia 97% mkoa huo ukishika nafasi ya pili huku mkoa wa Iringa ukiongoza kwa ushindi wa asilimia 98%. ambapo ushindi wa jumla kwa nchi nzima CCM kimeshinda kwa asilimia 81%, Katika mkutano huo pia Kinana amewaasa wana CCM kutotafuta mchawi  nje ya ila mchawi ni CCM wana CCM  wenyewe na akaongeza kwamba katika kujiandaa na uchaguzi mkuu ujao kigenzo muhimu kitakachoangaliwa sana ni uadilifu wa viongozi. 2Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Tangamano mjini Tanga. 3Umati Mkubwa uliohudhuria kwenye mkutano huo 4
Kutoka kushoto ni mwanamuziki Mzee Yusuf kiongozi wa bendi ya Taarab ya Jahazi na Mbunge wa jimbo la Korogwe vijijini Profesa Maji Marefu wakifuatilia mkutano huo.
5
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo katika mkutano huo.
6
Mwanamuziki Mzee Yusuf kiongozi wa bendi ya Taarab ya Jahazi akiwasalimia wananchi na mashabiki wake wakati wa mkutano huo wa hadhara.
7
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza  jambo na baadhi ya viongozi katika meza kuu kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh.Muhingo Rweyemamu
8
Mwanamuziki Mzee Yusuf kiongozi wa bendi ya Taarab na wanenguaji wake wakifanya vitu vyao jukwaani.
9
mwanamuziki Mzee Yusuf kiongozi wa bendi ya Taarab na wanenguaji wake wakifanya vitu vyao jukwaani.
11
Mh. Januari Makamba Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia akimpongeza mwanamuziki Mzee Yusuf mara baada ya kutumbuiza katika mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika kwenye viwanja vya Tangamano mjini Tanga.
12
Nyoomi ya kutosha
13
Aliyekuwa mgombea ubunge kupitia chama cha  CHADEMA Tanga mjini Bw. Hassan Omary Mbarak akitangaza rasmi kujiunga na CCM mara baada ya kupokea dozi ya kutosha kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu. Abdulrahman Kinana
14
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu. Abdulrahman Kinana akimpongeza Bw.Bw. Hassan Omary Mbarak kwa uamuzi wake wa kujiunga na CCM.
15
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu. Abdulrahman Kinana akiagana na wananchi mara baada ya kuhutubia mkutano huo wa hadhara kwenye viwanja vya Tangamano mjini Tanga.
16
Wengine walipanda juu ya magari kama wanavyoonekana
17
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Ndugu Henry Shekifu akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM ili kuongea na wananchi katika mkutano huo.
18
Baadhi ya mawaziri na viongozi mbalimbali wakiwa katika mkutano huo

No comments:

Post a Comment