Mratibu
 wa kituo cha TFGM na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Mtakatifu Catherine 
Laboure ya Kijiji cha Masanga kilichopo wilayani Tarime mkoani Mara, 
Thomas Maruga akiwatembeza maeneo mbalimbali ya shule hiyo na Mratibu 
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) na
 Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya 
watu duniani (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem (kushoto) wakati wa sherehe ya 
mahafali ya sita ya mabinti waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji (Waiseke 
wa Kisasa).
Na Mwandishi wetu, Tarime-Mara
SERIKALI imeombwa kuhakikisha inakomesha ubabe unaotumika kukeketa mabinti wa koo za Kikuria nchini.
Kauli
 hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kituo cha kupambana na ukeketaji cha 
Masanga, Tarime Sista Germaine Baibika akizungumza na waandishi wa 
habari baada ya kukamilika kwa sherehe ya mahafali ya sita ya mabinti 
waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji.
Alisema
 jumla ya mabinti 634 wamehitimu mafunzo ya miezi miwili yanayogusa haki
 za binadamu, haki zao, masuala ya afya na kuzitambua na kuezinzi mila 
nzuri.
Aidha wamejifunza kazi za sanaa na usanii.
Alisema
 adha kubwa wanayokumbana nayo mabinti hao waliotoka katika kituo hicho 
ni kukamatwa kwa nguvu na kupitishwa kisu cha Ngariba bila wao wenyewe 
kuafiki kwa dai la kuendeleza mila.
“Hii 
sio mila” anasema sista Germaine na kuongeza kuwa hakuna mila 
inayotengenezwa kunyanyasa watu wengine au kulazimisha mambo yasiyofaa 
katika jamii, mila hiyo ikiwepo lazima ipigwe vita.
Mgeni
 rasmi Waziri wa Kazi na Ajira, Mh. Gaudentia Kabaka (wa pili kushoto) 
akiwasili kwenye mahafali hayo pamoja na Mratibu Mkazi wa mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa 
Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto) aliyeambatana na 
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya 
watu duniani (UNFPA), Dkt Natalia Kanem.
Alisema
 serikali isiache kuwatetea mabinti hao kwa dai la kuwa hiyo ni mila kwa
 kuwa wanaofanyiwa vitendo hivyo hulazimishwa na haifanyiki kwa ridhaa 
yao.
Alisema
 wapo mabinti walioletwa na wazazi wao kuepushwa na janga hilo, wapo 
waliotoroka kwa wazazi wao na wapo walioletwa katika kituo hicho na 
polisi kutoka makwao.
Mafunzo
 hayo ya mwezi mmoja yamelenga kukabiliana na msimu wa ukeketaji ambao 
sisita huyo alisema mwaka jana ulianza mapema Novemba na unaendelea hadi
 mwaka huu wakati kimila mwaka huu si wa ukeketaji.
Kwa mujibu wa mila za Kikuria ukeketaji hufanyika katika mwaka unaogawanyika, mwaka 2015 haugawanyiki.
Mhashamu
 Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Mkoani Mara, Michael 
Msongazila akiwasili kwenye sherehe za mahafali ya sita ya kituo cha 
kupambana na ukeketaji Masanga wilayani Tarime mkoani Mara.
Mafunzo
 hayo ambayo yamelenga kuwatoa mabinti wa kisasa wenye mwelekeo wa 
maisha yenye hali bora mabinti wanaofika hapo huwa hawataki kukeketwa na
 ndio maana mwaka huu walipata tatizo la binti mmoja kuzimia wakati 
alipomuona baba yake katika maeneo ya kituo hicho.
Alisema
 wapo wazazi wakorofi wanaokuja kudai watoto wao lakini pia ipo jamii 
korofi inayotumia ubabe baada ya wasichana hao kutoka hapo wanakeketwa 
kwa lazima.
Katika
 hafla hiyo iliyoendeshwa na masista wa shirika la Daughters of Charity 
of St. Vincent De Paul, Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaudentia Kabaka 
aliwapongeza wasichana hao na kuwataka kuwa mfano katika jamii na 
kutekeleza wajibu wao.
Alisema wamekuwa mabinti wa kisasa kwa kukataa ukeketaji na hivyo wao wanastahili kuwa walimu kwa wenzao.
Maandamano
 ya wanafunzi wa Shule ya Mtakatifu Catherine Laboure iliyopo kijiji cha
 Masanga wilayani Tarime, mkoani Mara wakiwa na mabango yenye jumbe 
mbalimbali za kukemea ukeketeji wakisindikiza dada zao wahitimu wa kituo
 cha FGMT katika sherehe ya mahafali ya sita ya mabinti (Waiseke wa 
kisasa) waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji yaliyofanyika mwanzoni mwa 
wiki.
Aidha
 Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika
 la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez 
amewataka mabinti hao kuwa chachu ya mabadiliko katika jamii na kuwa 
chanzo cha kubadili kizazi kijacho.
Alisema wamesimama madhubuti kupinga mila potofu na uonevu na kusema kwa kitendo chao wamewafanya wengine kuwaiga na kubadilika.
Alisema
 ukeketaji ni mila potofu na kusema kwa msaada wa shirika la Umoja wa 
mataifa la Mpango wa familia (UNFPA) na taasisi nyingine zinazopambana 
na ukeketaji kwa kipindi cha miaka saba wamefanikiwa kuwoakoa wasichana 
2001 wasikeketwe.
Aidha mabinti hao wameokolewa dhidi ya ndoa za utotoni, ujauzito wa mapema na kushindwa kuendelea na masomo.
Naye
 Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya 
watu duniani (UNFPA), Dkt Natalia Kanem amesema ni vyema mapambano dhidi
 ya ukeketaji yakaendelea kwa kuwa wanaoshabikia ni viongozi wa kimila 
na ngumu kuiondoa ila kwa juhudi za jamii yenyewe.
Katika
 sherehe hizo ambapo pia askofu wa Musoma alikuwepo na viongozi wengine 
wa kiserikali pia Ngariba walioacha kazi hiyo walikuwepo kuelezea ubaya 
wa mila hiyo.
 Suala la ukeketaji ni kitu cha kawaida katika mikoa ya Manyara 71%, Dodoma 64%, Arusha 57%, Singida 51% na Mara 40%.
Viongozi
 waliopata muda wa kuzungumza walisema kwamba ukeketaji unatakiwa 
kukomeshwa mara moja kwani ni tatizo si tu kwa jamii bali kwa wale ambao
 wanafanyiwa kisaikolojia na kitabibu.
Wahitimu
 mabinti 37 waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji wa kituo cha TFGM cha 
kijiji cha Masanga wakiwasili na maandamano kwenye sherehe za mahafali 
ya sita ya kituo hicho.
Moja 
ya kazi inayoifanywa na kituo cha Masanga ni ushauri wa kisaikolojia 
kutokana na wasichana wengi kufika hapo wakiwa na matatizo makubwa ya 
magonjwa na hasa msongo wa mawazo.
Katika
 risala yao mabinti hao wameitaka serikali kufanyakazi yake kukabiliana 
na ubabe unaofanywa na viongozi wa kimila wa kuwalazimisha kukeketwa 
hata msimu unapokuwa umepita.
Mabinti
 hao ambao wengi wametoka shule ya msingi na sekondari wameweza kuwekwa 
hapo kwa msaada wa UNFPA ambao wametoa hela kupitia Children’s Dignity 
Fund (CDF), .Wafadhili wengine ni Daughters of Charity of St. Vincent Du
 Paul, na Askofu wa kanisa katoliki dayosisi ya Musoma, Michael 
Msongazila
Mgeni
 rasmi Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaudentia Kabaka akisalimiana na 
Mhashamu Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Mkoani Mara, 
Michael Msongazila mara baada ya kuwasili kwenye mahafali hayo.
Kwaya
 ya vijana ya mara ikiimba wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kwa sherehe za
 mahafali ya sita ya kituo cha kupambana na ukeketaji Masanga wilayani 
Tarime mkoani Mara.
Mgeni
 rasmi Mh. Kabaka, Bw. Alvaro Rodriguez na SSP. Simon Mrashani 
wakishiriki kucheza wimbo maalum unaohamasisha kukataza vitendo vya uovu
 vya Ukeketaji kwa watoto wa kike wakati wa mahafali hayo.
Mkurugenzi
 wa Kituo cha kupambana na ukeketaji cha Masanga (TFGM), Tarime, mkoani 
Mara, Sista Germaine Baibika akimkaribisha mgeni rasmi pamoja wageni 
waalikwa kwenye sherehe ya mahafali ya sita ya mabinti waliokwepeshwa 
msimu wa ukeketaji.
Mgeni
 rasmi Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaudentia Kabaka akifurahi jambo na 
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez kwenye 
sherehe za mahafali hayo.
Mgeni
 rasmi Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaudentia Kabaka akizungumza kwenye 
sherehe za mahafali ya sita ya mabinti waliokwepeshwa msimu wa 
ukeketaji.
Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akitoa 
salamu za Umoja wa Mataifa katika sherehe za mahafali sita ya mabinti 
waliokwepeshwa msimu wa ukeketaji.
Mkuu
 wa Wilaya ya Tarime, mkoani Mara, Bw. John Henjewele akitoa salamu kwa 
niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara katika mahafali ya sita ya kituo cha 
kupambana na ukeketaji cha kijiji cha Masanga (TFGM) cha wilayani 
Tarime, mkoani Mara.
Mwakilishi
 wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani 
(UNFPA), Dkt Natalia Kanem, akizungumza kwenye sherehe hizo.
Kaimu
 kamanda wa polisi wa kanda maalum ya Tarime na Rorya SSP. Simon 
Mrashani akieleza jinsi jeshi la polisi linavyoshiriki katika kupambana 
na masuala ya unyanyasaji wa kijinsia likiwemo suala la kesi za 
ukeketaji ambapo pia alitoa takwimu za kesi zilizoripotiwa kituoni mpaka
 sasa ni 141, huku 80 zikiwa Mahakamani na 20 zimetolewa hukumu.
Mtaalam
 wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce 
Temu akifurahi jambo na baadhi ya wafanyakazi wenzake wakati wa sherehe 
za mahafali hayo.
Wahitimu
 37 wakila kiapo cha kutokubali kutoshiriki kukeketwa na kuwa mabalozi 
wazuri kwenye jamii zao katika kuelemisha madhara ya ukeketaji kwa 
wanaoendeleza mila na tamaduni hizo pindi warudipo majumbani. Kwa picha zaidi ingia humu

No comments:
Post a Comment