TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, January 8, 2015

WENYEVITI MANYARA WAASWA KUWAONGOZA WANANCHI BILA KUWA NA UPENDELEO.

mmm
………………………………………………………….
WENYEVITI wa Vijiji, Vitongoji na Wajumbe wa Serikali za Vijiji wa Tarafa ya Moipo, Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wametakiwa kuwaongoza wananchi bila kuwa na upendeleo, huba, chuki, hofu, uoga na kuficha siri za ofisi.
Wito huo umetolewa juzi na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mirerani, Gofrey Haule, wakati akiwaapisha wenyeviti wa vijiji, vitongoji na wajumbe wa Serikali za vijiji wa Tarafa hiyo ili watunze siri za ofisi.
Hakimu Haule alisema ili jamii iweze kuwaamini viongozi hao wanatakiwa kutokwenda kinyume na maadili ya kazi, kutokwenda kinyume na utaratibu wao na bila kufanya kufanya upendeleo wowote kwa watu watakaowaongoza.
“Uongozi ni kama kuongoza njia hivyo mkijenga mahusiano mema kati yenu na jamii mtaweza kutekeleza majukumu yenu bila kuwa na shaka ila msikiuke viapo vyenu kwani siyo jambo jema mbele ya wananchi,” alisema Hakimu Haule.
Hata hivyo, baadhi ya viongozi walioapishwa waliahidi kuwa watawatumikia wananchi bila kuwa ubaguzi wowote ule, kwani hivi sasa suala la siasa lilishapita na kilichobaki ni kupambana na maendeleo ya jamii peke yake.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kiongoji cha Tenki la Maji, Rajab Msuya alisema wananchi wakishirikiana naye bega kwa bega wataweza kupiga hatua kubwa ya maendeleo kupitia fikra mpya na uongozi mpya uliopo eneo hilo.
Naye, Mwenyekiti wa kitongoji cha Kilimanjaro, Elizabeth Kisamo (Chadema) alisema atawatumikia wananchi wote wa kitongoji chake bila ubaguzi wa itikadi, dini, kabila au jinsia, kwani hivi sasa yeye ni kiongozi wa watu wote.
“Kwa sababu wazee ndiyo waliniomba niongoze hiki kijiji, nitajitahidi kuongoza kwa nguvu zangu zote ila busara zao bado ninazihitaji na waendelee kunipa ushirikiano wao,” alisema Mussa Chully, Mwenyekiti wa Kijiji cha Shambarai.

No comments:

Post a Comment