TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 6, 2015

WAPINZANI WATAKIWA KUTUMIA MAJUKWAA KUTANGAZA SERA ZAO NA SI KUTUKANA

imagesMWALIMUNa Mwamvua Mwinyi,Pwani

MBUNGE wa jimbo la Chalinze ,Bagamoyo mkoani Pwani ,Ridhiwani Kikwete amesema hayupo tayari kufanya mipasho ya kujibizana na baadhi ya viongozi kutoka upinzani, wanaokwenda kutukana na kubeza utekelezaji wa ilani ya CCM,kupitia mikutano ya hadhara katika jimbo hilo.
Amesema yeye ni mbunge wa kufikiria kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa jimbo hilo na sio kupoteza muda kwa kutukana majukwaani.
Akizungumza mara baada ya kufanya ziara yake kata ya Mdaula ambako vitongoji vinne vimechukuliwa na vyama vya upinzani katika uchaguzi uliopita,Ridhiwani alisema ifikie hatua kwa viongozi wa vyama kuacha kutumia mikutano ya wananchi kutoa matusi ama kejli kwa chama kingine na badala yake waseme masuala yenye tija.
Ridhiwani alieleza kuwa majukwaa ni moja ya fursa ya kueleza yale ambayo chama husika inayafanya, kuyatatua kwa wananchi na malengo yao ndani ya jamii na si kupoteza muda kubeza chama kingine ama kutoa dosari.
Alisema viongozi wote pasipo kujali itikadi za kisiasa wanatakiwa kuzungumza na wananchi kujua kero zao ,na namna ya kuzitatua badala ya kila kukicha kuzungumzia chama kingine ambacho kinaonekana utekelezaji wake.
Aidha Ridhiwani alisema ataendelea kuumiza kichwa kutafakari namna ya kupiga hatua kimaendeleo kwenye jimbo lake pasipo kujali itikadi za kisiasa.
“Kwa upande wangu,mimi,ni jukumu langu kusimamia na kushirikiana na wananchi wote kutekeleza yale wanayoyataka kwa kutafuta wadau na kuisukuma serikali kutekeleza  kero za wananchi ,na sitothubutu kuwa miongoni mwa wale ambao wanatenga jamii anayoiongoza kwasababu ya kisiasa’alisema Ridhiwani.
Aliwaomba wananchi kijumla na viongozi wa vyama vya upinzani walio katika maeneo machache ya jimbo la Chalinze kusema kero zinazowakabili,kumshauri na kumkumbusha kile atakachosahau ili waweze kushirikiana na hatimae kuinua maendeleo ya jimbo hilo.
Mbunge huyo anaendelea na ziara yake jimboni Chalinze,na tayari alishatembelea baaadhi ya vijiji na vitongoji kwenye kata za  Kibindu,Mbwewe,Ubena,Mdaula na Bwilingu.

No comments:

Post a Comment