MBUNGE
 wa jimbo la Chalinze ,Bagamoyo mkoani Pwani ,Ridhiwani Kikwete amesema 
hayupo tayari kufanya mipasho ya kujibizana na baadhi ya viongozi kutoka
 upinzani, wanaokwenda kutukana na kubeza utekelezaji wa ilani ya 
CCM,kupitia mikutano ya hadhara katika jimbo hilo.
Amesema
 yeye ni mbunge wa kufikiria kutatua kero mbalimbali zinazowakabili 
wananchi wa jimbo hilo na sio kupoteza muda kwa kutukana majukwaani.
Akizungumza
 mara baada ya kufanya ziara yake kata ya Mdaula ambako vitongoji vinne 
vimechukuliwa na vyama vya upinzani katika uchaguzi uliopita,Ridhiwani 
alisema ifikie hatua kwa viongozi wa vyama kuacha kutumia mikutano ya 
wananchi kutoa matusi ama kejli kwa chama kingine na badala yake waseme 
masuala yenye tija.
Ridhiwani
 alieleza kuwa majukwaa ni moja ya fursa ya kueleza yale ambayo chama 
husika inayafanya, kuyatatua kwa wananchi na malengo yao ndani ya jamii 
na si kupoteza muda kubeza chama kingine ama kutoa dosari.
Alisema
 viongozi wote pasipo kujali itikadi za kisiasa wanatakiwa kuzungumza na
 wananchi kujua kero zao ,na namna ya kuzitatua badala ya kila kukicha 
kuzungumzia chama kingine ambacho kinaonekana utekelezaji wake.
Aidha
 Ridhiwani alisema ataendelea kuumiza kichwa kutafakari namna ya kupiga 
hatua kimaendeleo kwenye jimbo lake pasipo kujali itikadi za kisiasa.
“Kwa 
upande wangu,mimi,ni jukumu langu kusimamia na kushirikiana na wananchi 
wote kutekeleza yale wanayoyataka kwa kutafuta wadau na kuisukuma 
serikali kutekeleza  kero
 za wananchi ,na sitothubutu kuwa miongoni mwa wale ambao wanatenga 
jamii anayoiongoza kwasababu ya kisiasa’alisema Ridhiwani.
Aliwaomba
 wananchi kijumla na viongozi wa vyama vya upinzani walio katika maeneo 
machache ya jimbo la Chalinze kusema kero zinazowakabili,kumshauri na 
kumkumbusha kile atakachosahau ili waweze kushirikiana na hatimae kuinua
 maendeleo ya jimbo hilo.
Mbunge huyo anaendelea na ziara yake jimboni Chalinze,na tayari alishatembelea baaadhi ya vijiji na vitongoji kwenye kata za  Kibindu,Mbwewe,Ubena,Mdaula na Bwilingu.

No comments:
Post a Comment